• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mafunzo ya matumizi ya mfumo mpya wa ununuzi wa Umma (NeST) yaanza rasmi Mkoani Morogoro.

Posted on: August 28th, 2023

 

Washiriki wa mafunzo ya  Mfumo mpya wa kielektroniki wa Manunuzi ya Umma (National e - Procurement System of Tanzania NeST) Mkoa wa Morogoro wametakiwa kujifunza na kuelewa vema Mafunzo hayo ili kwenda kufundisha Maafisa wengine mara watakapo rejea Katika Halmashauri zao hususan Wakuu wa Idara kwa lengo la kuanza kukutumia Mfumo huo ifikapo Oktoba mwaka huu


Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimali watu Bw. Herman Tesha akizungumza na washiriki wa mafunzo ya matumizi ya mfumo mpya wa Ununuzi wa Umma (NeST).

Wito huo umetolewa na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimali watu Herman Tesha Leo Agosti 28, 2023 alipokuwa anafungua mafunzo ya NeST yaliyofanyika Katika Ukumbi wa mikutano wa Mbaraka Mwishehe uliopo katika Manispaa ya Morogoro.

Pichani ni baadhi ya washiriki wa mafunzo ya Mfumo mpya wa Ununuzi wa Umma (NeST) wakimsikiliza mwezeshaji wa mafunzo hayo Bw. Steven Benedict.

Mafunzo hayo ni mwendelezo wa kuwajengea uwezo wataalam wa Idara mbalimbali ngazi ya Halmashauri hapa nchini juu ya matumizi sahihi ya mfumo mpya wa manunuzi (NeST) uliozinduliwa na Serikali Julai 1 mwaka huu ambapo Mkoani Morogoro yameanza kutolewa rasmi hii Leo  Agosti 28.

Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Katibu Tawala WA Mkoa wa Morogoro Dk. Mussa Ali Mussa Bw. Herman Tesha amewataka washiriki hao wa mafunzo  kutumia kikamilifu muda huo kuelewa vyema Mafunzo hayo ili kusaidia Mkoa huo kutumia Mfumo huo kuanzia mwezi Oktoba mwaka huu.

Aidha, imeagizwa kuwa hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa kwa wale watakao fanya manunuzi ya umma nje ya Mfumo wa NeST.

Afisa Tehama kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw. Herman Njelekela akiwaelekeza washiriki wa mafunzo hayo jinsi ya kutumia mfumo huo.

Mwaka 2019 Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) ilianzisha mfumo wa kielektroniki wa manunuzi ujulikanao kama Tanzania National e-Procurement System (TANePS) kwa lengo la kuhakikisha kuwa Taasisi za Serikali zinatumia mfumo huo katika uendeshaji wa michakato ya ununuzi wa umma.

Bw. Steven Benedict ambaye ni Mkaguzi wa Ndani kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akitoa mafunzo kwa washiriki wa mafunzo ya Mfumo mpya wa Ununuzi wa Umma (NeST).

Mmoja wa wawezeshaji wa mafunzo ya mfumo mpya wa Ununuzi wa Umma (NeST) Bw. Leopold Ngirwa akifananua mambo mbalimbali kuhusu mfumo huo.

Aidha, Serikali ilibaini uwepo wa changamoto mbalimbali katika mfumo wa TANePS hivyo, Mwezi Julai mwaka huu ilianzisha mfumo mpya wa manunuzi wa National e-Procurement System of Tanzania (NeST) ili kukidhi mahitaji ya Nchi katika manunuzi ya umma na kukabiliana na changamoto za mfumo wa TANePS.

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Utawala na Rasilimali watu Bw. Herman Tesha (wanne kutoka kushoto waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na wawezeshaji  na washiriki wa mafunzo hayo kutoka baadhi ya Halmashauri za Mkoa huo baada ya ufunguzi wa mafunzo hayo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.