• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mafunzo ya Sensa ya Watu na Makazi.

Posted on: July 24th, 2022

Washiriki wa Sensa ya Watu na Makazi wafundwa

Washiriki wa Sensa ya watu na Mkazi ngazi ya Mkoa Mkoani Morogoro wanaoendelea kunolewa kwa siku 21, wametakiwa kuwa wazalendo pindi watakapokwenda kutoa mafunzo hayo kwa Makalani wa Sensa katika ngazi za Wilaya.



Baadhi ya Washiriki wa Sensa ya watu na Mkazi ngazi ya Mkoa Mkoani Morogoro wakiendelea na mafunzo yao yanayofanyika katika kituo cha kutolea Elimu ya watu wazima (WAMO) Mkoani humo.

Rai hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa morogoro Mhandisi Ezron Kilamuhama alipowatembelea washiriki hao kwa lengo la kuangalia maendeleo ya mafunzo hayo yanayofanyika Kituo cha kutolea Elimu ya Watu Wazima (WAMO) kilichopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Akiwa katika eneo la mafunzo Mhandisi Ezron Kilamuhama amesema zoezi la Sensa ya watu na Makazi hufanyika mara moja kila baada ya miaka 10, kwa sababu hiyo washiriki wanatakiwa kuwa makini katika kufundisha walio chini ambao ni  ngazi ya Wilaya.

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Ezron Kilamuhama akizungumza na Washiriki wa Sensa ya watu na makazi (Hawapo Pichani).

Amebainisha kuwa endapo kutakuwa na makosa yoyote yatakayofanyika katika sense ya mwaka huu na kwa kuwa sense hufanyika kila baada ya miaka kumi basi makosa hayo yataathiri taifa na wananchi wake kwa miaka kumi ijayo, hivyo pamoja na changamoto zozote zitakazojitokeza wakati wa zoezi hilo ni budi watangulize nidhamu na Uzalendo kwa taifa lao.

“lakini pamoja na hayo niwaombe sana kwa sababu kama nilivyotangulia kusema lina umuhimu wa kipekee na ni zoezi la kitaifa, lazima tujitahidi sana kuwa walimu, tulifanye kwa nidhamu kubwa sana lakini pia tulifanye kizalendo” amesisitiza Mhandisi Kilamuhama.

Hata hivyo, amesema sense ya mwaka huu ni ya kipekee ukilinganisha sensa ya miaka mingine kwa kuwa sensa ya mwaka huu kwanza ni inafanyika kidijitali lakini pia inahusisha Makazi na ndio maana imetanguliwa na zoezi la Anwani za Makazi na Posti kodi ambapo Mkoa wa Morogoro ulitekeleza zoezi hilo kwa 106% ya lengo, jambo ambalo litarahisisha sana zoezi lote la Sensa ya watu na Makazi.

Mmoja wa wawashiriki wa mafunzo ya Sensa  ya watu na makazi akijikumbusha namna ya kutumia zana ya kukusanyia Takwimu kidijitali (Kishikwambi) kitakacho tumika wakati wa Sensa hiyo.

Naye Mratibu wa Sensa Mkoa wa Morogoro Bw. Charles Mtabo amesema mafunzo hayo ya sensa ngazi ya Mkoa yanahusisha washiriki takribani 416 na yameanza Julai 6 na yatakamilika Julai 26, 2022 na baada ya kukamilika wataanza ngazi ya tatu ya mafunzo hayo ya sensa ambayo ni ya ngazi ya Wilaya.

Mratibu wa Sensa ya watu na Makazi Mkoa wa Morogoro Bw. Charles Mtabo.


Kwa upande wake Roda Sheba ambaye ni mshiriki, amesema madhumuni ya Serikali kuwa na sensa ya watu na Makazi ni kupata takwimu sahihi zitakazosaidia serikali kupanga mipango yake ya kuwahudumia wananchi,hivyo akatoa wito kwa wananchi, kwanza kujiandaa kushiriki sensa hiyo lakini pia kutoa takwimu zilizo sahihi huku akitoa rai kwa washiriki wenzake kuwa wazalendo wakati wote wa zoezi la Sensa.

Roda Sheba ambaye ni mmoja wa washiriki wa Sensa ya watu na makazi Mkoa wa Morogoro ametoa wito kwa washiriki wenzake kuwa wazalendo wakati wote wa zoezi hilo.

Sensa kwa maendeleo,  jiandae kuhesabiwa

MWISHO 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.