• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Malima aagiza viongozi wa REA, TANESCO kusimamia kwa karibu zaidi miradi inayotekelezwa Mkoani humo.

Posted on: July 25th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amemuagiza Meneja wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoani humo kusimamia miradi kwa karibu miradi inayotekelezwa Mkoani humo ili iweze kukamilika kwa wakati na kwa ubora unatakiwa.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akizungumza na wadau wa sekta ya nishati wakati wa kikao cha kupokea taarifa ya ya REA na TANESCO.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo Julai 24 mwaka huu wakati wa kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa miradi ya REA na TANESCO Mkoani humo, kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Mhe. Adam Malima amesema, Serikali imetoa fedha nyingi za kutekeleza miradi ya usambazaji umeme katika Mkoa huo ili kuondoa changamoto ya upatikanaji wa umeme kwa wananchi wake jambo ambalo bado linakwamishwa na wakandarasi wachache kutofikia malengo hayo.

Kwa sababu ya wakandarasi hao kuchelewesha kukamilika kwa miradi hiyo kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa inapelekea wananchi kuitupia lawama Serikali yao, hivyo ameagiza viongozi wa REA na TANESCO Mkoa wa Morogoro kuwasimamia wakandarasi kukamilisha miradi hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Adam Malima akiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa wakati wa kikao.

“...hebu tuangalie hili suala la monitoring and supervision kwa wakandarasi wetu ili pale ambapo serikali imepeleka fedha na miradi inatakiwa kukamilika kwa wakati basi ikamilike...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Akitolea mfano Mkandarasi M/s HNXJDL JV ambaye anatekeleza mradi usambazaji umeme vijijini wenye thamani zaidi ya shilingi bilioni 26 katika Wilaya za Kilosa, Mvomero na Gairo miradi 78 iliyotakiwa kukamilika Disemba 2022 lakini hadi sasa Mkandarasi huyo amewasha umeme katika vijiji 27 pekee, hivyo ameongezewa muda hadi Disemba 2023 kukamilisha vijiji vilivyobaki hali ambayo bado inaleta wasiwasi kama atakamilisha miradi yote kwa huo uliobaki.

Sambamba na hilo, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka Meneja wa REA na TANESCO Mkoani humo kushirikiana na Jeshi la Polisi kudhibiti wizi wa miundombinu ya umeme katika Mkoa huo ikiwemo mafuta ya Transifoma na nyaya za shaba.

Pamoja na kushirikiana na Jeshi hilo, Mkuu wa Mkoa amemwagiza Meneja wa TANESCO kutafuta mbinu mbadala za teknolojia za kisasa za kuwakamata wezi wa miundombinu ya umeme ikiwa ni pamoja kuwa na vifaa vinavyorekodi matukio hayo katika maeneo mbalimbali hususan yaliyokithiri matukio hayo.

Naye, Meneja wa TANESCO Mkoani Morogoro Mhandisi Fadhili Chilombe ameeleza mikakati ya Shirika hilo ya kuhakikisha Mkoa wa Morogoro unaondoa au kupunguza changamoto ya upatikanaji wa umeme ndani ya Mkoa huo.

Miongoni mwa mikakati hiyo ni pamoja na kununua transifoma mpya ya MV 120 ambayo itazalisha umeme Megawati 102 na kwamba kwa sasa wapo katika hatua ya ufungaji wa transifoma hiyo katika kituo cha kupoozea umeme cha Msamvu na wanatarajia kazi hiyo kukamilika ifikapo Oktoba 31 mwaka huu, hivyo changamoto ya kukatika umeme katika Manispaa ya Morogoro itapungua.

Meneja wa TANESCO Mkoa wa Morogoro Mhandisi Fadhili Chilombe akielezea mikakati ya shirika hilo ndani ya Mkoa huo.

Ameongeza kuwa shirika la TANESCO limetenga Bilioni 4.6 kwa ajili ya matengenezo ya njia za kusambaza umeme pamoja ununuzi wa nguzo za zege 551 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya umeme.

Kwa upande wake Mhandisi wa Miradi ya REA Mkoani Morogoro, Bi. Aneth ameeleza changamoto zinazoikabili REA katika majukumu yake zikiwemo idadi ya wananchi wanaojitokeza kuunganishwa ni ndogo japokuwa bei ni 27,000 katika maeneo ya vijijini, changamoto ya miundo mbinu ya barabara katika baadhi ya Wilaya hivyo kusababisha ucheleweshwaji wa vifaa.

Meneja miradi ya REA Mkoa wa Morogoro Mhandisi Aneth Malingumu akiwasilisha taarifa ya miradi ya REA inayotekelezwa Mkoani humo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.