• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Malinyi itatoboa bilioni 4 ndani ya mwaka mmoja na nusu - Mhe. Adam Malima.

Posted on: June 7th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adamu Kighoma Malima amesema endapo Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi watakubaliana kusimamia makusanyo ya mapato ya ndani, Halmashauri hiyo ina uwezo wa kukusanya zaidi ya shilingi Bilioni Nne ndani ya mwaka mmoja badala ya kukusanya shilingi bilioni 2.5 kwa mwaka.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (kushoto) akiwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Malinyi Mhe. Pius Mwelase wakati wa kikao.

Mhe Adam Malima amebainisha hayo Juni 6 mwaka huu wakati wa kufungua Mkutano Maaluma wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi kwa ajili ya kujadili hoja za Mkaguzi Mkuu wa Serikali - CAG.
Mkuu huyo wa Mkoa amesema Wilaya ya Malinyi ni moja ya Wilaya zilizojaaliwa ardhi nzuri na yenye rutuba ambayo kwayo inaweza kustawisha kila aina ya zao na kwamba malinyi inaweza kulisha mchele Tanzania nzima.
amesema kama Halmashauri ya Malinyi wataamua kwa dhati kukusanya mapato ya ndani, wana uwezo wa kukusanya zaidi ya shilingi Bilioni 4 kwa mwaka, kinachohitajika ni usimamizi.


"Kama Halmashauri hii tutakaa na tukakubaliana kufanya kazi ya usimamizi, Malinyi tutatoboa bilioni 4 ndani ya mwaka mmoja na nusu au miwili" amesema Mhe. Adam Malima.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro Ndg. Solomon Kasaba akitoa salam za chama hicho wakati wa mkutano wa madiwani.

Aidha, amewataka Madiwani wa Halmashauri hiyo kusimama kidete katika kuwekeza kwenye kilimo cha mazao ya kimkakati yakiwemo zao la michikichi na karafuu.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Malinyi Mhe. Pius Mwelase akizungumza kwenye mkutano wa Baraza la Madiwani Wilayani humo.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kushughulikia vema hoja za CAG na kuwataka kukamilisha hoja zilizosalia ili kuiweka halmashauri hiyo katika nafasi nzuri zaidi.

Hawa ni baadhi ya Waheshimiwa Madiwani katika Halmashauri ya Malinyi waliohudhuria mkutano huo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.