• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MARUFUKU KUAGIZA MBEGU NJE YA NCHI - DKT. MPANGO.

Posted on: May 27th, 2021

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango amezitaka kampuni zinazoagiza mbegu kutoka nje ya nchi kuzalisha mbegu hizo hapa nchini kutokana na tija ndogo inayopatikana kupitia sekta ya kilimo  na kuitaka Wizara ya Kilimo kusimamia utekelezaji wa maelekezo hayo.

Kauli hiyo ameitoa Mei 27, 2021 wakati akihitimisha maadhimisho ya kumbukizi ya 17 ya hayati Edward Moringe Sokoine yaliyofanyika Mkoani Morogoro  katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo – SUA ambapo alikuwa mgeni rasmi wa maadhimisho hayo.

‘’Ninazitaka kampuni zote zinazoagiza mbegu kutoka nje zizalishe mbegu hizo hapa nchini na Wizara ya Kilimo ijipange kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa maelekezo haya, taasisi zetu za Magereza na JKT lazima zijizatiti zaidi katika uzalishaji wa mbegu’’ Amesema Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango amesema kutokuwepo kwa hatua madhubuti za kuinua sekta ya kilimo kumepelekea kushindwa kushawishi viongozi, vijana na wasomi kujikita katika kilimo biashara na kutofanikiwa kuzishawishi taasisi za kifedha kutoa mikopo yenye riba nafuu katika sekta ya kilimo.

Katik hatua nyingine, Dkt. Mpango ameitaka Wizara ya Kilimo na Mifugo kufikisha huduma za ugani kwa wakulima  vijijini na kusimamia mfumo mzima wa vitendea kazi kuwafikia wakulima hao ili kuwanufaisha na kilimo hicho.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo hicho Jaji Mstaafu Joseph Warioba amebainisha lengo mahususi la kuanzishwa kwa Chuo hicho ni kufanya tafiti na kuwajenjea uwezo wanafunzi  kujitegemea kwa kupiga vita umasikini na kutoa huduma zinzohitajika kwenye kilimo kwa wananchi wa vijijini.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Martine Shigela amesema atashirikiana vizuri na SUA katika kukuza uzalishaji wa kilimo kwa kutimiza zima ya Serikali ya Mkoa huo kuwa ghala la chakula kwa kufanya mapinduzi ya sekta ya kilimo na kuenzi mazuri ya hayati Moringe Sokoine.

Hayati Moringe Sokoine alifarikii Aprili 12, 1984 eneo la Dakawa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro, ambapo kumbukizi ya mwaka huu inatimiza miaka 37 tangu kufariki kwake ikibebwa na kaulimbiu ‘’ Teknolojia za Kilimo, Tija na Ushindani katika Soko: Tanzania kuelekea Nchi ya Uchumi wa Kati wa Juu.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.