• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MBIO ZA MAGARI MOROGORO KUTANGAZA UTALII

Posted on: September 20th, 2025



Mashindano ya mbio za magari yaliyozinduliwa leo Mkoani Morogoro yanatarajia kwenda kuutangaza Utajiri wa Mkoa huo hususan utalii wa mbuga za Wanyama, milima ya Udzungwa na utajiri mwingine uliopo ndani ya Mkoa huo.

Hayo yamebainishwa leo Septemba 19, 2025 na Waziri mwenye dhamana ya Michezo, Sanaa na Utamaduni  Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi wakati akifungua mashindano hayo katika viwanja vya Kiwanda cha Tumbaku cha Mkwawa Leaf Mkoani Morogoro.

Amesema, mashindano hayo ya mbio za Magari yanayojulikana kama Mkwawa Rally of Tanzania (African Rally of Championship) yanakwenda kutoa mchango mkubwa katika kuutangaza Utalii wa Mkoa wa Morogoro hivyo kukuza Uchumi wake na wa Taifa la Tanzania.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema, Mkoa wa Morogoro una vigezo lukuki vya kuwa mwenyeji wa mashindano hayo ikiwa ni Pamoja na uzuri wa mazingira yanayovutia, Usalama na uwezo wake kuratibu matukio makubwa kama hayo.

Aidha, ameishukuru Serikali kwa kuunga mkono na kuuendeleza mchezo huo huku akiwashukuru wananchi wa Morogoro kushiriki uzinduzi wa mbio hizo za magari na ametumia fursa hiyo kuliomba Shirikisho la mchezo huo Duniani, kuuleta tena mchezo Mkoani humo na kuahidi kuwa watajipanga na kufanya vema zaidi kuliko mwaka huu.

“Tumeongea nao watu wa shirikisho ili mwakani wailete tena tujipange na kuwa kitu kikubwa kwa hapa Morogoro na kwa Tanzania” amesisitiza Mhe. Adam Malima.

Naye Yohana Emmanuel Manu kwa niaba ya wananchi wa Mkoa huo amesema, mashindani hayo yanaleta hamasa, umoja na Ushirikiano miongoni mwa watanzania na ndugu zetu wa nchi Jirani, lakini pia amesema mashindano hayo yanaongeza watalii hivyo kukuza Uchumi wa mtu mmoja mmoja kupitia bidhaa wanazouza na kuongeza mzunguko wa fedha ndani ya mkoa.

Mashindano hayo ya African Rally of Championship yatafanyika kwa siku tatu kuanzia Septemba 19 hadi Septemba 21, 2025 na kushirikisha wanamichezo kutoka nchi za Kenya, Unganda, Rwanda India na wenyeji Tanzania.



MWISHO 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Morogoro kuanzisha jarida la programu ya PJT–MMMAM

    September 30, 2025
  • Viongozi wa Serikali Mkoani Morogoro watakiwa kulinda UHAI wa Bonde la Kilombero.

    September 26, 2025
  • Gairo kuanza kuhamasisha kilimo biashara.

    September 25, 2025
  • Gairo kuanza kuhamasisha kilimo biashara.

    September 25, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.