• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Meneja TARURA Kilombero kuchukuliwa hatua kwa kutokamilisha ujenzi kwa wakati

Posted on: October 5th, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amesema Ofisi yake itamchukulia hatua za kinidhamu Meneja wa Wakala ya Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Wilaya ya  Kilombero kwa kutosimamia kikamikifu ujenzi wa barabara ya Kibaoni – Nanganje kwa kiwango cha lami yenye urefu wa mita 900 baada ya muda wa kukamilisha ujenzi huo kupita.

Dkt. Mussa ametoa agizo hilo Oktoba 4 mwaka huu alipotembelea mradi huo kuona hatua iliyofikiwa wakati wa ziara yake ya siku moja ya kukagua miradi ya barabara katika Wilaya za Kilombero na Ulanga.

Amesema, Serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 400 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo, na muda wa kukamilika ilikuwa Septemba 30, 2023 kwa sababu hiyo Meneja huyo anapaswa kuchukuliwa hatua kwa kile alichokiita ni uzembe katika kutekeleza majukumu yake.


 "...kuna haja ya kuwachukulia hatua wahusika wa TARURA kwa sababu wao ndiyo waliomtafuta mkandarasi, wao ndiyo waliosimamia... na barabara yenyewe haifiki hata kilometa moja na fedha zipo, kila kitu kipo lakini bado barabara haijamalizika...” amesema Dkt. Mussa.


Aidha, Katibu Tawala huyo amemtaka Meneja huyo wa TARURA kuhakikisha kuwa kazi zake anazozisimamia zinakamilika kwa wakati na kwa kiwango kinachotakiwa kulingana na fedha iliyotolewa ili kuwasaidia wananchi watakaotumia barabara hiyo kuondokana na changamoto ya ubovu wa barabara.


Naye, Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Morogoro Ndg. Solomon Kasaba amesema ucheleweshaji wa miradi ya barabara inasababisha wananchi kuitupia lawama Serikali na chama cha CCM kuwa haifanyi kazi, wakati kuna watu wachache tu ndiyo kikwazo cha kugombanisha wananchi na Serikali yao huku akishauri TARURA kuchukua wakandarasi wenye sifa ili kukidhi mahitaji ya miradi husika.


Kwa upande wake Meneja wa TARURA Wilayani Kilombero Mhandisi Kalume amesema sababu ya kutokukamilika kwa wakati kwa mradi huo ni pamoja na kuchelewa kupatikana kwa msamaha wa kodi, mvua hasa kipindi cha masika, pamoja na uwezo mdogo wa kifedha wa mkandarasi anayejenga barabara hiyo. 


Ujenzi wa barabara hiyo ya Kibaoni - Nanganje utakaogharimu shilingi mil.400 hadi kukamilika kwake umefikia asilimia 60, na mkandarasi ameshalipwa shilingi Mil. 200. 


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.