• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MENEJA WA SHULE YA SEKONDARI YA GREEN CITY MKOANI MOROGORO ASIMAMISHWA KAZI

Posted on: January 10th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa ameagiza uongozi wa shule ya Green City iliyopo katika Manispaa ya Morogoro kumsimamisha kazi Bwana Henri Wadelanga (60) kwa kosa la kumpiga hadi kupoteza fahamu mwanafunzi Asia Haidari Sharifu wa kidato cha tano mchepuo wa HGK katika shule hiyo.

Mhe. Fatma Mwassa ametoa agizo hilo Januari 10 mwaka huu alipotembelea shule hiyo kwa ajili ya kutoa uamuzi na kuzungumza na walimu pamoja na wanafunzi wa shule hiyo.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Bwana Henri Wadelanga amefanya makosa mbalimbali yakiwemo kumpiga mwanafunzi hadi kupoteza fahamu, kinyume na sheria kwa kuwa yeye sio mwalimu hivyo haruhusiwi kupiga wanafunzi.


Sambamba na hilo, Mkuu wa Mkoa amemuagiza Afisa Elimu Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na Mganga Mkuu wa Mkoa kumpeleka mwanafunzi huyo Hospitali ya Rufaa ya Mkoani hapa  ili kubaini kama amepata athari nyingine za kiafya zilizotokana na kipigo hicho.

Akithibisha kutokea kwa tukio hilo Afisa Elimu Mkoa wa Morogoro Bi. Germana Mung'aho amesema tukio hilo limetokea tarehe 8 Januari mwaka huu majira ya saa tatu usiku ambapo Meneja huyo alikuwa anawapokea wanafunzi waliotoka likizo.

Afisa Elimu huyo ameongeza kuwa Ndugu Henri Wadelanga alichukua hatua hiyo ya kumpiga mwanafunzi huyo kwa madai ya kwamba alitukanwa na mwanafunzi huyo.

Aidha ameongeza kuwa tukio Hilo limeshafunguliwa jarada   (Morogoro RB No. 228/2023) katika kituo Kikuu cha Polisi Mkoani Morogoro na mtuhumiwa anashikiliwa na vyombo vya dola kwa hatua zaidi za kisheria.

Sambamba na hilo Bi. Germana Mung’aho ametoa wito kwa walimu juu ya utoaji wa adhabu kwa wanafunzi kwa kufuata Waraka wa Elimu kuwa hauruhusu mwanafunzi kupigwa maeneo mbalimbali ya mwili wake, na adhabu ya viboko ndiyo adhabu kubwa inayotambulika.

Aidha Waraka huo wa Elimu umewataka walimu kutoa adhabu ya viboko isiyozidi vinne na lazima Mwalimu Mkuu au Mkuu wa shule aidhinishe na iwekwe kimaandishi kwenye kitabu cha adhabu.

Kaka wa mwanafunzi huyo Bwana Yasin Sharifu amesema changamoto ya usafiri ndiyo iliyopelekea wao kuchelewa kufika kwa wakati katika shule hiyo, lakini walitoa taarifa kwa Mwalimu Mkuu wa shule na kupata kibali.

Kufuatia maelekezo ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro mwanafunzi huyo amepelekwa Hospaitali ya Rufaa Mkoani hapa ili kubaini kama amepata athari nyingine za kiafya zilizotokana na kipigo hicho.

MWISHO.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.