• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mhe. Mwanyika aridhishwa na mpango wa mazao matano ya kimkakati Morogoro.

Posted on: February 15th, 2025

Mwenyekiti wa  Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deo Mwanyika (MB) amefurahishwa na mpango madhubuti wa utekelezaji wa mazao ya kimkakati Mkoani ili kuhakikisha kuwa sekta ya kilimo inaboresha maisha ya wanamorogoro na watanzania kwa ujumla.

Mhe. Deo Mwanyika amesema hayo Februari 15, Mwaka huu wakati wa ziara ya kamati hiyo Mkoani Morogoro ambapo siku ya kwanza ya ziara  hiyo imetembelea Vitalu vya miche ya parachichi na shamba la viazi mviringo katika vijiji vya  Mkogwe na Masenge Wilayani Gairo.

Akifafanua zaidi, Mwenyekiti huyo amesema Mkoa huo umefanikiwa kuanzisha mpango wa kilimo cha mazao biashara kama Parachichi, Karafuu, Kokoa, Michikichi na Kahawa ili kuhakikisha wakulima wanazalisha kwa tija na kuinua uchumi wao.


"... Mhe. Rais ameongeza bajeti ya kilimo mara 100 kutoka tsh. Bil. 270 na tunaongelea sasa Trilioni 1.1 na itaongezeka zaidi..." amesema Mhe. Deo Mwanyika.


Aidha, amewahimiza wananchi kupanda miti sambamba na zao la parachichi ili kusaidia kuhifadhi mazingira na kuhakikisha upatikanaji wa mvua ya kutosha kwa kilimo kwani bila miti hali inaweza kusababisha ukame na kurudisha nyuma kilimo hicho.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema kuwa Mkoa huo unahakikisha mapinduzi makubwa ya kilimo hasa cha mazao hayo matano na kwa upande wa Wilaya ya Gairo yanaongezeka mazao ya viazi na Tumbaku mkakati unaolenga kuhimili mabadiliko ya tabianchi lakini pia kuondoa dhana ya watanzania walio wengi kuwa kilimo hakina tija.


Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa, amebainisha kuwa Wilaya ya Gairo hususan sehemu za milimani ina hali ya hewa inayofaa kwa zao la parachichi na viazi mviringo na kwamba  wanashirikiana na taasisi mbalimbali kufanikisha mkakati huo ikiwa ni pamoja na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) ambayo imeandaa miche 100,000 ya parachichi  na kutoa bure kwa wakulima kwa ajili ya kupanda katika mashamba yao.

Wakati huo huo, Diwani wa Kata ya Chagongwe Mhe. Frank Robert Kyangala ameishukuru Serikali kwa kutoa elimu kwa wakulima ili kuongeza tija ya uzalishaji katika kilimo na kuondoa umaskini katika kata yake huku akiiomba Serikali kuwajengea barabara kwa kiwango cha lami inayotoka Gairo hadi Tarafa ya Nongwe ili kurahisisha usafirishaji wa mazao kwenda sokoni.


Nao wakazi wa Kijiji cha Mkobwe katika Tarafa ya Nongwe akiwemo Bi. Neema Mnjowe ambaye ni mwanachama wa Kikundi cha Mboto kinachojishughulisha na uandaaji wa miche ya parachihi na miti ya mbao amesema wamepata mafunzo ya kuotesha mbegu za parachichi na miti ya mbao ili kumebadilisha maisha yao na kujikimu mahitaji yao muhimu yakiwemo mavazi, malazi na chakula.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.