• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mhe. Mwanyika atoa wito wafanyabiashara kuimarisha Mfumo wa Stakabadhi Ghalani.

Posted on: October 21st, 2024


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deodatus Mwanyika ( Mb) ametoa wito kwa wafanyabiashara kushirikiana na Serikali kwa kutoa taarifa kwa mamlaka husika mara wanapoona watu wenye nia ovu ya kudhoofisha Mfumo huo.

Mhe. Deodatus ametoa wito huo Oktoba 20, 2024 wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo iliyofanyika Wilayani Mvomero Mkoa wa Morogoro yenye lengo la kukagua na kujadili mustakabali wa mazao mbalimbali ya biashara likiwemo zao la Kakao na kusisitiza matumizi ya mfumo wa Stakabadhi Ghalani.

Akifafanua zaidi, Mwenyekiti huyo amesema wafanyabiashara wengi hupata maslahi yao binafsi kwa kutofuata taratibu za manunuzi ya mazao kwa wananchi hivyo amewasisitiza kutoa taarifa ili hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

".. Mimi nitoe wito tutoe ushirikiano ili tuimarishe huu mfumo, kama tunajua kuna watu wanafanya ujanja ujanja tutoe taarifa kwa wakati kwa viongozi wetu.." amesisitiza Mhe. Deodatus Mwanyika.

Kwa sababu hiyo, Mwenyekiti huyo  ameielekeza Bodi ya Stakabadhi za Ghala (WRRB) kueneza mfumo huo katika mikoa yote hapa nchini pamoja na kuongeza idadi ya mazao kutoka kwa wakulima huku akiwataka kufanya kazi kwa bidii na ubunifu ili mfumo huo ufanye kazi kikamilifu na kumnyanyua mkulima.

Sambamba na hayo, Mhe. Mwanyika ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wakulima na kuboresha maisha yao kwa kuwaletea mfumo huo ambao unawasaidia wakulima kuuza mazao yao kwa bei ya elekezi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe (MB) amewataka wakulima kuendelea kujituma, kufanya kazi kwa bidii na kutumia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kwa manufaa yao ili kuinua kipato chao na Taifa kwa ujumla.

Nao wakulima wa Mhonda juu akiwemo Boli Paul Ndege amesema mfumo huo unawasaidia kuweka ile bei elekezi na kuwanufaisha ambapo ni tofauti na hapo awali hakukuwa na ya matumizi ya mfumo huo kwani wakulima walikuwa wakiuza mazao yao kwa bei ya chini.

MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.