• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MHE. SIMBACHAWENE AWATAKA WAAJIRI KUTENGA BAJETI KUSHIRIKI MICHEZO YA SHIMIWI.

Posted on: October 5th, 2024

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na utawala bora Mhe. George Simbachawene (MB) amewataka Waajiri wa watumishi wa umma kutenga bajeti itakayowawezesha watumishi hao kushiriki mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) kuanzia hapo mwakani.

Mhe. Simbachawene ametoa agizo hilo Oktoba 5, Mwaka huu Mkoani Morogoro wakati akifunga mashindano ya SHIMIWI yaliyofanyika katika viwanja  mbalimbali vya michezo  vilivyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Aidha, Waziri huyo amesema kuwepo kwa upungufu wa vilabu kutoka 74 mwaka 2023 hadi vilabu 66 mwaka 2024 ni ishara isiyofaa kwa watumishi wa Umma, hivyo amewataka waajiri watambue umuhimu wa michezo hiyo ili kuanzia mwaka 2025 watumishi wengi washiriki michezo hiyo.

"... nitumie nafasi hii kutoa maelekezo kwa waajiri wote wa watumishi wa umma, kuhakikisha wanatoa fedha za kutosha kwenye mipango na bajeti ili kuwezesha ushiriki wa watumishi katika michezo ya SHIMIWI..." Amesema Mhe. George Simbachawene.

Waziri Simbachawene amesema michezo hiyo inajenga afya ya akili, mwili pamoja na kuepusha magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama presha, ugonjwa wa Moyo, mfumo wa upumuaji, mzunguko wa damu, kuimarisha misuli na kuongeza ufanisi wa utendaji kazi wa mwili.


Aidha, Mhe. Simbachawene ametumia fursa hiyo kuwataka watumishi hao wa umma kwa upande wao kufanya kazi kwa bidii katika maeneo yao ya kazi kwa kutoa huduma bora kwa wananchi

Akiongea kuhusu uchaguzi, Waziri huyo amewaagiza Makatibu Wakuu, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakuu wa Sehemu na Vitengo kuhakikisha wanajiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura ili kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, Mwaka huu kwani amesema watumishi hao wamekuwa na kasumba ya kutoshiriki chaguzi hizo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema Mkoa huo unasifika kwa michezo kutokana na Amani iliyopo ambayo ndio chachu ya maendeleo na kuwashukuru wanamichezo wa SHIMIWI kwa kufanya utalii wa kutembelea Mbuga za Mikumi, hifadhi ya Mwalimu Nyerere na Udzungwa pamoja na vivutio vingine vilivyopo ndani ya Mkoa huo.

Mwenyekiti wa SHIMIWI Taifa Bw. Daniel Mwalusamba ameishukuru Wizara ya Utamaduni, Sanaa, na Michezo kwa kutoa miongozo iliyosaidia kufanikisha usimamizi wa michezo hiyo na kwamba pamoja na jukumu hilo bado wameshiriki kwenye masuala kijamii ambapo wametembelea vituo vya kulea watoto yatima ndani ya Manispaa ya Morogoro na kutoa vifaa mbalimbali kulingana na uhitaji.

Michezo hiyo ya 38 tangu kuanzishwa kwake imejumuisha wanamichezo 20995 ambapo wanaume  ni 1683 na wanawake ni 1312 kutoka katika Wizara 20, Mikoa 19, Wakala wa Serikali 3 na Taasisi za Umma 14.

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.