• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mhe.Fatma Mwasa Asisitiza Lishe Bora Mkoani Morogoro.

Posted on: August 6th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa amesema kwa kutambua kuwa lishe bora ni kichocheo katika Nyanja zote za maendeleo, Serikali imeazimia kufanya tathmini ya kila mwaka kuhusu hali ya lishe na tathmini maalum ya kila baada ya miaka mitano kwa lengo la kuhakikisha kuwa taifa linakuwa na wananchi wenye afya bora na wenye uwezo wa kuchangia shughuli za maendeleo.

Fatma Mwassa amesema hayo Agosti 5, 2022 mwaka huu wakati wa kikao cha tathmini ya nusu Mwaka cha Lishe ngazi ya Mkoa kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo ikiwa ni kikao chake cha kwanza kujadili masuala ya lishe tangu ateuliwe kuongoza Mkoa huo.

Akifafanua zaidi Mkuu huyo wa Mkoa amesema ili Mkoa uweze kukabiliana na utapiamlo inatakiwa mikakati  na mipango thabiti yenye lengo la kuwekeza katika lishe na kuhakikisha shilingi 1000 ambazo Halmashauri zilielekezwa kutenga kutoka katika vyanzo vyao vya mapato kwa ajili ya kuboresha lishe kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano zinatengwa na kutumika kwa nia hiyo. 

Kwa upande wake Afisa Lishe wa Mkoa wa Morogoro Salma Magembe amesema Mkoa bado unakabiliwa na tatizo la udumavu kwa kiasi kikubwa, kwani pamoja na takwimu kuonesha tatizo hilo linapungua kutoka asilimia 33.4 2015/2016 hadi asilimia 26.4 mwaka 2018 bado Mkoa huo una idadi watoto laki moja mia saba na thelathini wenye udumavu.

Hata hivyo Bi.Salma amesema Mkoa umejipanga kutatua changamoto hiyo kwa kutoa Elimu kuhusu utumiaji wa vyakula kwa watoto huku akibainisha kuwa Mkoa wa Morogoro una vyakula vingi vya aina tofauti tatizo ni Elimu ya namna ya kupangilia kutumia vyakula hivyo eneo ambalo amesema linatakiwa kuwekewa mkazo zaidi kupitia watendaji wa Serikali wa ngazi mbalimbali.

Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mkoani Humo Mathayo Masele yeye anatoa wito kwa watendaji wote wa Serikali zikiwemo Ofisi za Wakuu wa Wilaya kuendelea kushirikiana na Ofisi za Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri katika kuhamasisha wananchi ili kuondokana na suala la utapiamlo na udumavu kwa watoto.

Nao washiriki wa kikao hicho akiwemo Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mlimba Simoni Mkali amewataka wananchi kuondokana na mila potofu zinazochangia udumavu kwa watoto, ikiwemo ya kumwaga maziwa ya mama anayoyatoa saa moja baada ya kujifungua kwa kuamini kuwa ni maziwa hayo ni machafu jambo ambalo sio sahihi.



MWISHO

                                                  

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.