• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MIAKA 61 YA UHURU WATANZANIA WAJIVUNIA MAENDELEO.

Posted on: December 9th, 2022

Wadau wa maendeleo Mkoani Morogoro wamesifu hatua za maendeleo ambayo nchi ya Tanzania imefikia ukilinganisha na hali ya nchi hiyo wakati inapata uhuru ambapo nchi ilikuwa katika hali isiyoridhisha kimaendeleo.

Sifa hizo zimetolewa Disemba 9 mwaka huu na wadau mbalimbali kwenye Mdahalo wa kujadili maendeleo endelevu ambayo Halmashsuri ya Manispaa ya Morogoro imefikia katika kipindi cha miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania, mdahalo huo umefanyika kwenye ukumbi wa mikutano uliopo Manispaa ya Morogoro.

Miongoni mwa wadau hao ni Bw. Deograsias Mhaiki ambaye ni Afisa Elimu Taaluma Manispaa ya Morogoro amesifu maendeleo yaliyopatikana katika sekta ya elimu ambapo hapo awali shule zilikuwa chache na nafasi ya wanafunzi kuchaguliwa kujiunga na shule za sekondari ilikuwa ni nadra sana.

Aidha, ameongeza kuwa kwa sasa katika Manispaa hiyo wanafunzi wanapata nafasi ya kujiunga na elimu ya sekondari kwa kuwa shule ni nyingi takribani 29, hata changamoto ya vyumba vya madarasa kwa sasa imepungua, pia hakuna chaguzi tatu kama ilivyokuwa hapo awali.

Kwa upande wake Bw. Jeremiah Lubeleje Mchumi wa Manispaa ya Morogoro amepongeza juhudi kubwa iliyofanyika katika kuboresha miundombinu hapa nchini na amesema watanzania wanasababu ya kujivunia katika hilo kwa sababu kuna baadhi ya nchi kama vile msumbiji wananchi wake waishio mipakani wamekuwa wakifuata huduma za afya nchini Tanzania.

Sambamba na hilo Mchumi huyo amewashauri vijana ambao wamehitimu elimu ya sekondari na vyuo vikuu hapa nchini kutokubweteka badala yake wajishughulishe na shughuli mbalimbali ikwemo kilimo au ufugaji kwa lengo la kujikwamua kutokana na changamoto ya ajira.

Bi. Amina Rashid mwandishi wa habari kutoka kituo cha Planet Redio amesema kuna mabadiliko makubwa katika teknolojia ya habari na mawasiliano ambapo kwa sasa watu wanapata taarifa na matukio kutoka maeneo mbalimbali hapa duniani kupitia simu zao za viganjani, tofauti na hapo awali wakati nchi inapata uhuru redio, televisheni na simu zilikuwa chache hivyo taarifa zilikuwa zinachelewa kuwafikia watu.

Nae Bw. Bakari Nsulwa ambaye alikuwa mwenyekiti wa mdahalo huo wakati akihitimisha majadiliano amesema watanzania wanatakiwa kuendelea kudumisha Amani, umoja, na mshikamano tulionao kwani ndiyo silaha pekee katika mustakabali wa maendeleo ya Taifa letu.

Aidha mwenyekiti huyo amesisitiza watanzania kuwa wazalendo na nchi yao kwani hata mataifa makubwa yameimarika kutokana na wananchi wake kuwa wazalendo kwa nchi zao.

Kwa upande wake Bw. Silas Ikanga ambaye ni Mhasibu wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mkoani Morogoro amesema watanzania wanapaswa kumuenzi Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius kambarage Nyerere kwa kupinga ukabila, udini, pamoja na ukanda, hata hivyo amesisitiza wanamorogoro kuishi maono na fikra za Mwalimu Nyerere.

Uhuru wa Tanganyika ulipatikana mnamo Disemba 9 mwaka 1961, kutoka kwa waingereza na Mwalimu J. K. Nyerere alikuwa Waziri Mkuu wa kwanza.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.