• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Michezo ni nyezo ya kupambana na uharifu, madawa ya kulevya - Makamu wa pili wa Rais Zanzibar.

Posted on: September 6th, 2024

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema michezo ni moja ya nyenzo muhimu hapa nchini katika kupambana na uharifu na matumizi ya madawa ya kulevya.

Makamu wa Pili wa Rais amesema hayo Septemba 6, 2024 Mkoani Morogoro wakati akizindua mashindano ya Michezo ya Majeshi hapa nchini yaliyoratibiwa na Baraza la Michezo ya Majeshi ya Tanzania (BAMMATA) na kufanyika katika uwanja wa Jamhuri uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro yakiwa na lengo la kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana.

Mhe. Hemed Suleiman amesema,  michezo inasaidia katika kupambana na kuzuia uharifu na matumizi ya madawa ya kulevya ndani ya jamii kwa njia ya kuwashawishi wananchi hususan vijana kujiunga kwenye michezo ili kuepusha kujiingiza kwenye vitendo viovu hususan ubakaji, wizi, ujambazi na matendo mengine yasiyokubalika katika jamii.

"...mara kadhaa tumekuwa tukitumia michezo kama nyenzo ya kupambana na uharifu na matumizi ya madawa ya kulevya kwa kuwashawishi vijana kujiunga kwenye michezo..." amesema Mhe. Hemed Suleiman

Aidha, Makamu huyo wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema, michezo inajenga afya ya akili, mwili pamoja na kuepusha magonjwa mbalimbali yakiwemo presha, Moyo na mfumo wa upumuaji  ndani ya majeshi na kwa wananchi kwa ujumla.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa BAMMATA Brigedia Jeneral Said Hamisi  Said amesema mashindano hayo yatafanyika kwa siku 10 kuanzia Septemba 6 hadi 15, 2024 na kutaja michezo itakayochezwa katika mashindano hayo kuwa ni mpira wa Miguu, mpira wa mikono, mpira wa kikapu, mpira wa wavu, mchezo wa riadha, mchezo wa ngumi, mchezo wa vishale na kulenga shabaha

Sambamba na hayo amebainisha Viwanja vitakavyotumika kwenye mashindano hayo ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuwa ni viwanja vya Jamhuri, viwanja vya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine - SUA, viwanja vya chuo cha Kijeshi cha Pangawe na viwanja vya Bwalo.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.