• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Migogoro yapungua Morogoro – RAS Morogoro

Posted on: January 2nd, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo amebainisha kuwa migogoro ya Ardhi katika Mkoa huo imepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na Serikali ngazi ya Taifa,  Mkoa pamoja na Wilaya kwenda kutatua migogoro hiyo moja kwa moja kwenye maeneo husika.

Mhandisi Kalobelo amebainisha hayo hivi karibuni Ofisini kwake alipokuwa anaongea na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Angelina Mabula alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja Mkoani humo.

Amesema Migogoro iliyobaki sasa ni ile ya Wananchi wachache kuwa na tabia ya kuvamia hifadhi za Taifa na sio migogoro baina ya mtu na mtu au baina ya jamii ya wakulima na wafugaji ambayo ilisumbua sana miaka ya nyuma.

Amebainisha kuwa sababu kubwa ya kupungua kwa migogoro hiyo ni pamoja na baadhi ya Wilaya kupitiwa na Mradi wa urasimishaji wa Ardhi uliojulikana kama Land Tenure support Programme katika Wilaya za Ulanga, Malinyi na Kilombero ambapo vipande vyote vya ardhi vya Wilaya hizo vilirasimishwa hivyo kupunguza migogoro ya Ardhi.

Sababu nyingine ni Viongozi wa Serikali katika ngazi zote kutumia muda mwingi kwenda kutatua kero hizo kwenye tukio badala ya kutatua migogoro hiyo kuwa Ofisini jambo ambalo pia limesaidia kupata ukweli zaidi na kuondoa pengine kutatua migogoro pasipo kuona ukweli na uhalisia.

“Mkoa wa Morogoro ulionekana kama ni Mkoa wa Migogoro ya Ardhi, lakini kwa Ushirikiano na Wizara yako nipende kusema migogoro imepungua sana kutokana na hatua mbalimbali ambazo zimekuwa zikichukuliwa” alisema Mhandisi Kalobelo.

Aidha, ameongeza kuwa uamuzi wa Serikali wa kuwabadilishia vituo vya kazi Maafisa wa Ardhi wa Mkoa wa Morogoro kwa wakati mmoja na kuwaleta Maafisa wengine wapya umechangia kupunguza kero kwa kuwa zoezi hilo liliongeza uwajibikaji kwa maafisa Ardhi hao wapya kwa kutekeleza majukumu yao ya kikazi kikamilifu (commitment).

Kuhusu wananchi kuendelea kuvamia hifadhi, Kalobelo amesema tayari Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amekwisha litolea maelekezo suala hilo kuhakikisha maeneo yote ya hifadhi Mkoani humo yanalindwa kwa mujibu wa sheria zilizopo.

Kwa upande wake Naibu Waziri Angelina Mabula pamoja na kupongeza hatua za Mkoa kupunguza migogoro ya Ardhi amesema ni muhimu Elimu iendelee kutolewa kwa wananchi waliorasimishiwa ardhi zao na kupewa hati miliki za kimila kwa ajili kuendeleza uchumi wa familia zao kwa kuzitumia hati hizo kupata mikopo katika taasisi za kibenki kwa kuwa zinatambulika.

Aidha, amesema Wilaya ambazo zina mashamba pori yaliyofutiwa umiliki wake, zitatakiwa kufanya maandalizi ya matumizi ya mashamba hayo mara Mkoa utakapopokea maelekezo ya Serikali, Wilaya hizo zinatakiwa kujipanga na kuwa na Mpango wa matumizi sahihi ya mashamba hayo ambayo Serikali itawajulisha muda mchache ujao.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.