• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MJADALA WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA WAHITIMISHWA

Posted on: November 2nd, 2022

MJADALA WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA WAHITIMISHWA, MOROGORO YAAZIMIA..


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Abubakar  Mwassa akifuatilia mjadala wa Nishati safi ya kupikia kwa njia ya mtandao (mubashara) kutoka Dar es Salaam


Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa akiweka kumbukumbu sahihi yale machache aliyopata kwenye mjadala huo


Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Mathayo Massele akihitimisha mjadala wa nishati safi ya kupikia Mkoani Morogoro kwa niaba ya Mkuu wa MKoa huo 




Baadhi ya Wahe. Wakuu wa Wilaya wakifuatilia kwa makini Mjadala wa Nishati Safi ya kupikia


wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri wakifuatilia mjadala huo

Baadhi ya Wajumbe wa Sekretarieti ya Mkoa wakishiriki pia mjadala wa nishati safi ya kupikia

Makatibu Tawala wa Wilaya ya Malinyi na Ulanga wakifuatilia mjadala kwa umakini mkubwa, ni ukweli usiopingika mjadala huu umewagusa watu wengi

Mjadala wa siku mbili uliohusu Nishati safi ya kupikia ambao umeandaliwa na Wizara ya Nishati, kufanyika Jijini Dar es Salaam na Mikoa mingine ya Tabora, Dodoma, Iringa, Shinyanga na Morogoro kushiriki kwa njia ya mtandao umetamatika Novemba 2 mwaka huu.

Mkoa wa Morogoro wenyewe umeazimia suala hilo la Nishati safi ya kupikia iwe ni ajenda ya kudumu, kuendelea kuzungumzwa kwenye vikao vyote vya kisheria kwa lengo la kutafuta mbinu mbadala lakini pia kutoa uelewa kwa wananchi wake kuhusu madhara ya matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia.

Kauli ya azimio hilo imetolewa na Mhe. Mathayo Maselle Mkuu wa Wilaya ya Malinyi kwa niaba ya Mkuu wa MKoa huo Mhe. Fatma Abubakar Mwassa alipokuwa anafunga mjadala huo hapa Mkoani Morogoro na kuwashukuru wadau mbalimbali kwa kushiriki mjadala huo muhim uliofanyika katika hoteli ya Morena Mjini Morogoro.

“...Jambo hili tunaposubiri maelekezo muhim, basi tuifanye kama ajenda ya kudumu, kila mahali tunapokwenda kwenye mikutano yetu katika ngazi ya Wilaya ngazi ya Kata na ngazi za Vijiji iwe ajenda ya kudumu tuizungumze...” ameagiza Mhe. Mathayo Maselle.

Jijini Dare es Salaam, akihitimisha mjadala huo Waziri wa Nishati Mhe. January Makamba amesisitiza namna atakavyotekeleza Maagizo ya Mhe, Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoyatoa Novemba 1 mwaka huu wakati akifungua mjadala huo.

Baadhi ya maagizo hayo ni pamoja na kuunda kikundi kazi kitakachohusika  au shughulikia Nishati Safi ya Kupikia, kuanzisha mfuko wa Nishati Safi ya Kupikia na kuondoa wavamizi wote wa vyanzo vya maji hususan katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.

Bw. Aristotle James Afisa Masoko wa kampuni ya Viridium Tanzania Limited akitoa maelezo kwa washiriki namna ya kutumia majiko na nishati  ya mkaa mweupe ambao unazalishwa na Kampuni hiyo.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Miundombinu Mkoa wa Morogoro Mhandisi Ezron Kilamhama (kulia) akipokea jiko la kupikia na mkaa mweupe kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Malinyi ambavyo  ni salama na havina madhara kwa mazingira na binadamu

Afisa Wanyama Pori Mkoa wa Morogoro Joseph Chuwa (kulia) akipokea jiko la kupikia linalotumia mkaa mweupe, tayari kwa matumizi ya nishati safi ya kupikia

baadhi ya washiriki kutoka katika taasisi mbalimbali za Serikali na za binafsi walishiriki kikamilifu mjadala huo hapa Morogoro

 MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.