• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

M/KITI MASUNGA AIAGIZA RUWASA KUKAMILISHA MRADI WA MAJI WA IGAWA

Posted on: September 28th, 2024

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Morogoro Mhandisi Joseph Masunga amewaagiza Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Malinyi kukamilisha ujenzi wa mradi wa maji wa kata ya Igawa ifikapo oktoba 30 mwaka huu.

Mhandisi Masunga ametoa agiza hilo septemba 28, mwaka huu wakati wa ziara ya wajumbe wa kamati ya siasa ya Mkoa huo kutembelea baadhi ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya Mkoa leo wakiwa Wilayani Malinyi ili kujionea hatua ya miradi ilipofikia na ubora wake.

Akitoa agizo hilo, Mwenyekiti huyo amesema mradi huo wenye thamani ya Tsh. Milioni 855 ulipaswa kukamilika Julai 7, 2022 hivyo, amewataka watendaji wa RUWASA kukamilisha mradi huo haraka ili kutatua kero ya upatikanaji wa maji kwa wakazi 18674 waliopo katika vijiji vitatu vya Igawa, Lugala na Kiwale.

"… unatakiwa ukamilishe mradi kwa wakati kama ulivyoahidi hapa, wananchi waanze kupata maji katika kata ya Igawa…" amesema Mhandisi Joseph Masunga.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Joseph Masunga amewataka wahandisi wa ujenzi wa barabara ya Itete Njiwa hadi Ipera itakayogharimu Tsh. Mil. 266  kukamilisha mradi huo kwa wakati huku akimtaka msimamizi wa mradi huo uliofikia 65% amlipe kwa wakati mkandarasi ili aweze kutekeleza vema mkataba wake na maagizo anayopewa.

Sambambana hayo, Mwenyekiti Masunga ameipongeza serikali ya awamu ya sita ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji thabiti katika sekta ya elimu ukiwemo ujenzi wa shule ya msingi wa Misegese na kuwapongeza wasimamizi wa mradi huo kwa kusimamia maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Malinyi Mhandisi Marco Chogero amebainisha kazi zinazoendelea kufanyika ni ujenzi wa fensi eneo la tanki, uchimbaji na ulazaji wa mabomba na ujenzi wa vituo vya kuchota maji huku akiahidi kazi hizo zote kukamilika kabla au ifikapo Oktoba 30, 2024 kama ilivyoagizwa.

Naye Diwani wa Kata ya Igawa Mhe. Sevalius Kamguna amesema amefurahishwa na ujio wa kamati ya siasa wilayani humo kwani amesema inaongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kupitia maelekezo yanayotolewa na Kamati hiyo.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.