• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MKoa wa Morogoro kujitathmini kwenye kilimo

Posted on: November 30th, 2020

Wilaya za Mkoa wa Morogoro kupitia Halmashauri zake zimetakiwa kufahamu na kujiwekea malengo yakilimo kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2020/2021 katika kuzalisha mazao ya Biashara na ya chakula ili mwisho wa msimu huo zifanye tathmini kujua kama Wilaya na Mkoa kwa ujumlaunasonga mbele kwa upande wa sektahiyo ya Kilimo ama unarudi nyuma.

Maagizo hayo yametolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo Novemba 26 mwaka huu wakati wa maadhimisho ya uzinduzi wa Msimu wa Kilimo 2020/2021 yaliyofanyika Kimkoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba Wilayani Kilombero Mkoani humo.

Mhandisi Kalobelo alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Loata Ole Sanare,amesemaMkoa wa Morogoro ni Mkoa wa Kilimo na ni Ghala la chakula la Taifa, hivyo kuna kila sababu ya kuchukua hatua za makusudi katika kuendeleza Sekta ya kilimo ili heshima ya Morogoro kuwa ghala la chakula iwe na maana.

Mhandisi Kalobelo amesema, lengo la agizo hilo ni kutaka kujua malengo waliyojiwekea kwa kila Wilaya kama yametekelezwa au ayakutekelezwa na sababu zilizopelekea kutotekelezwa malengo hayo hatua ambayo itasaidia kujua mwelekeo wa sekta ya  kilimo ndani ya Mkoa.

“hakikisheni kila Wilaya inafahamu malengo yake ya msimu wa mwaka 2021 kwa upande wa mazao ya chakula na mazao ya biashara ….kwa sababu ya kufanya hivyo ni kutaka kujua kama tunakwenda mbele au tunarudi nyuma”alisema Mhandisi Kalobelo.

Sambamba na maagizo hayo, Mhandisi Kalobelo amewataka Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Mkoa huo kuhakikisha wanaweka utaratibu mzuri wa kutoza ushuru wa mazao ya kilimo kwa wakulima au wafanyabiashara wanaosafirisha mazao hayo kwa lengo la kuepuka kuwatoza ushuru huo zaidi ya mara moja na kwamba hilo litafanikiwa endapo wataimarisha mawasiliano kwa Halmashauri zinazopakana.

Katika hatua nyingine MhandisiKalobelo amewapongeza Viongozi wa Wilaya ya Kilombero pamoja na Halmashauri ya Mlimba Wilayani humo kwa kutoa Mkopo wa zaidi ya shilingi milioni 820kwa vikundi 99 vya wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu ikiwa ni mkopo usio na ribawafedha zinazotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo kuanzia Mwezi Julai hadi Oktoba mwaka huu.

Amesema huo ni mfano wa kuigwa kwa halamashauri nyingine za Mkoa huo huku akiwataka waliopata Mkopo huo usio na riba kuhakikisha wanarejesha fedha hizo kwa wakati ili wengine waweze kukopeshwa lakini pia wametakiwa kupitia fedha hizo kuanzisha miradi yenye tija.

Ili kuhakikisha vikundi hivyo vinapata tija, Mhandisi Kalobelo amewataka Wataalamu katika Halmashaurizote kuvisaidia vikundi katika kuandika Maandiko ya miradi yenye tija kwa vikundi vyenyewe, kwa jamii na taifa kwa ujumla huku akibainisha kuwa hilo ndilo lengo la Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ulanga Ngollo Malenya mmoja wa Wakuu wa Wilaya walioshiriki maadhimisho hayo, aliwataka wanawake kuendelea kuwa waaminifu kwenye mikopo ya fedha za Serikali kwa kuwa wameonekana ni waaminifu zaidi katika marejesho ya fedha hizo ukilinganisha na wanaume.

Aidha, kuhusu uzinduzi wa kilimo Ngollo Malenya amesema amejifunza mengi katika sherehe hizo ikiwa ni pamoja na mbinu mpya za kilimo cha umwagiliaji cha zao la mpungahususan kupanda zao la mpunga kkwa kutumia mafungu.

Naye, Katibu Tawala Msaidizi Mkoani humo, anayeshughulikia masuala ya kilimo Dkt. Rozalia Rwegasira pamoja na kuwakumbusha wakulima kuwa msimu w kilimo umeanza huku akiwataka wakulima kutambua kuwa kilimo ni Biashara kama zilivyo biashara nyingine hivyo ni wajibu wao kukithamini na kukienzi, kulima kwa malengo na kufuata kanuni bora za kilimo.

Aidha, aliwakumbusha Maafisa Kilimo kuanza kuandaa ratiba ya kuwatembelea wakulima na kutoa ushauri unaohitajika  ili wakulima waweze kuzalisha kwa tija na kwamba maafisa kilimo hawahitajika kukaa Ofisini hususan katika kipindi hiki cha kilimo.

Baadhi ya Wakurugenzi walioshiriki maadhimisho hayo akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo  Agnes Mkandya amesema maadhimisho hayo yamemwongezea ujuzi huku akiahidi akipendezwa na kilomo cha zao la kokoa linalolimwa katika halmashauri hiyo na kwamba ameazimia pia zao hilo kulimwa katika halmashauri ya Gairo.

Maadhimisho hayo ya uzinduzi wa Msimu wa Kilimo Mkoani Morogoro ambayo kwa mwaka huu yalikuwa na kaulimbiu “Kilimo endelevu kwa lishe Bora, Ajira na Maendeleo ya Viwanda”Mwakani yanategemewa kufanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Wilayani Morogoro.

 

MWISHO

 

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.