• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mkoa wa Morogoro kuwa kitovu cha uchumi wa Tanzania.

Posted on: November 14th, 2023

Mkoa wa Morogoro umejipanga kukuza uchumi wa Mkoa na nchi kwa ujumla kwa kujikita kwenye sekta ya kilimo chenye tija, ufugaji wa kisasa pamoja na kuhifadhi mazingira.

Hayo yamebainishwa Novemba 13 mwaka na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima wakati akifungua kikao cha wadau wa kilimo, mifugo na mazingira Mkoa wa Morogoro kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Morena iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akizungumza na wadau wa kilimo wakati wa kikao cha wadau wa kilimo, mifugo, uvuvi na mazingira Mkoa wa Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Mkoa wa Morogoro unaendelea na jitihada za kuhifadhi na kulinda mazingira kwa kuwa ni kichocheo cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii hapa nchini. Aidha, amesema utunzaji wa mazingira hususan vyanzo vya maji ndani ya Mkoa huo utawahakikishia upatikanaji wa umeme kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere ambalo linatarajia kuzalisha Megawati zaidi ya 2,000.

“...wao wajue jinsi ambavyo sisi Morogoro tunavyopigana kuhifadhi na kutunza mazingira kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya Taifa hili... lazima sisi watu wa Morogoro tulinde vyanzo vya maji na kuhifadhi mazingira...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Kwa upande wa sekta ya kilimo, Mkuu wa Mkoa amesema Mkoa huo  umepanga kuzalisha mazao ya biashara likiwemo zao la parachichi, ambapo wakulima 20 na Maafisa ugani wataenda Mkoa wa Njombe kupata mafunzo ya zao hilo na watapatiwa miche ya parachichi 50,000 kwa ajili ya kupandwa katika Tarafa ya Nongwe Wilayani Gairo.

Sambamba na hayo, Mhe. Adam Malima amewahimiza wakulima wa Mkoa huo kujiunga kwenye vyama vya ushirika ili waweze kupatiwa mikopo na pembejeo za kilimo zikiwemo mbolea, mbegu na zana za kulimia kutoka Taasisi za mikopo za Mkoa huo.

Kwa upande wake Meneja wa taasisi ya Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania – SAGCOT Mkoa wa Morogoro Bw. James Banga amesema kikao hicho cha wadau wa Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Mazingira kimelenga kufanya mapitio ya maazimio ya kikao kilichofanyika 2022 ili kuboresha utunzaji wa Mazingira, kilimo chenye tija kinacholinda mazingira pamoja na uvuvi bora.

Aidha, ameongeza kuwa hali ya utunzaji wa Mazingira katika Mkoa huo imeimarika kutokana na nguvu kubwa ya usimamizi wa viongozi wa Mkoa huo pamoja na utayari wa Wananchi katika kulinda mazingira kwa kuhamasika kulima mazao ya viungo mbalimbali ambayo hayaharibu mazingira.

Nao baadhi ya wakulima akiwemo Mwenyekiti wa vyama vya ushirika – AMCOS za miwa Bonde la Kilombero Bw. Bakari Mkangamo amewaasa wakulima kujiunga na vyama vya ushirika ili kupata urahisi wa pembejeo za kilimo pamoja na mikopo.

Wajumbe wa kikao hicho wameazimia mambo mbalimbali ikiwemo Mkoa kujikita kwenye kilimo cha mazao ya viungo likiwemo zao la karafuu huku Mkoa ukisaini hati ya makubaliano ya kiutendaji na Asasi za kiraia na Sekta binafsi kwa ajili ya kufanya mapinduzi ya kilimo hususan kilimo mazao, mifugo, uvuvi na mazingira.

 


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.