• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUTANGAZA VIVUTIO/ KUKUZA UTALII.

Posted on: July 27th, 2024

MKOA WA MOROGORO WAJIPANGA KUTANGAZA VIVUTIO/ KUKUZA UTALII.


Serikali Mkoani Morogoro kwa sasa inajipanga kwa ajili ya kuweka mazingira na mikakati madhubuti ya kutangaza vivutio vilivyopo mkoani humo kwa lengo la kukuza Sekta ya Utalii na kuingizia mkoa huo na taifa kwa ujumla mapato yatokanayo na sekta hiyo.


Hayo yamebainishwa Julai 26, 2024 na Afisa Maliasili wa Mkoa huo Bw. Joseph Chuwa wakati wa kikao cha wadau mbalimbali  wa utalii kilichofanyika Ofisi ya  Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ili kujadili na kuandaaa kongamano la wadau wa utalii wa Mkoa huo.


Bw. Chuwa amesema, katika kikao hicho wameweka mikakati ya kuhamashisha utalii kupitia makala ya Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaani Royal Tour ambayo imeleta uhai mkubwavkatika sekta ya utalii hiyo itasaidia Mkoa wa Morogoro uliobarikiwa vivutio vingi vya utalii kufadika kimapato kwa faida ya wanamorogoro na watanzania wote kwa jumla.


".. Lengo letu hapa ni kuweka mkakati wa kuona namna gani tunatumia fursa hizi pia mkakati wa kuona namna gani  tutaweza kutumia vivutio tulivyonavyo ili kufungua utalii ndani ya Mkoa ..." Amesema Bw. Joseph Chuwa.


Aidha Bw. Chuwa ametoa wito kwa Sekta binafsi Mkoani humo kuchangamkia fursa ya ujio wa treni ya kisasa (SGR) ambayo itatumika sana kuleta watalii wengi ndani ya Mkoa huu hivyo wananchi wawekeze katika mahoteli makubwa ya kitalii yatakayoweza kutoa huduma nzuri kwa wageni.


Kwa upande wake Balozi wa Utalii Tanzania ambae pia ni  Mkurugenzi wa NABEC Company limited  Bi. Nangasu Warema katika kikao hicho amesema kuna umuhimu wa Wanamorogoro kutambua faida ya utalii hivyo kama Sekta ya utalii ina jukumu la kutoa elimu kwa wananchi hao juu ya faida ya utalii na kuweza kujihusisha katika Sekta hiyo ili kujiingizia kipato na kukidhi maisha yao.


Naye,  Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi kanda ya Mashariki ( TANAPA) Bw. Fedrick Malisa katika hatua ya kukuza utalii Mkoani humo ametoa ushauri wa kuweka video fupi katika treni ya kisasa (SGR) pia katika mabasi kwa lengo la kuvitangaza vivutio vilivyopo Mkoani humo ili kuweza kuwavutia watalii kwa wingi.


Sambamba na hayo mdau kutoka kampuni ya SEE AFRICA SATARIS Bi. Eda Kapinga amesema Serikali ya Mkoa ina umuhimu wa kujikita katika Sekta ya utalii ambapo itawashawishi na kuleta chachu kwa wananchi wa Mkoa huo kujihusisha katika masuala ya utalii.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.