• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MKUU WA MKOA WA MOROGORO ATOA MAAGIZO KIWANDA CHA KILOMBERO.

Posted on: April 24th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ameutaka Uongozi wa Kiwanda cha Sukari cha Kilombero kushughulikia malalamiko ya wakulima wanaopeleka miwa yao katika kiwanda hicho ikiwemo madai ya ucheleweshwaji wa kuvuna zao hilo jambo ambalo linatajwa kurudisha nyuma jitihada za wakulima hao.

Shigela ameyasema hayo April 23, mwaka huu wakati wa mkutano na Uongozi wa Kiwanda cha Sukari cha Kilombero, Viongozi wa vyama vya ushirika vya wakulima wa miwa, wakulima wa zao la miwa Pamoja na viongozi wa Halmashauri za Wilaya ya Kilosa na Kilombero uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Sukari Cha  Kilombero.

Shigela ameutaka Uongozi wa Kiwanda hicho kuhakikisha miwa inayolimwa na wakulima hao  inachukuliwa na kiwanda hicho na pasiwepo na miwa inayotupwa.

“nielekeze Uongozi wa Kiwanda ufanye kinachowezekana kuchukua miwa ya wakulima. Sitarajii mwaka huu kuona tena miwa inatupwa, Kama kiwanda kina uwezo wa kuchukua kiasi cha miwa kilicholimwa basi uwekwe utaratibu kiasi hicho chote kichukuliwe ”. Amesema Shigela.

Akifungua Mkutano huo, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wakulima wa miwa katika bonde la Kilombero kumweleza bila kificho changamoto zinazowakabili katika kilimo hicho ili kuondosha malalamiko kati yao na Kiwanda cha Sukari Kilombero jambo ambalo linaweza kuzorotesha uzalishaji wa zao hilo.

Wakiongea mbele ya Mkuu huyo wa Mkoa baadhi ya wakulima wa zao hilo wamesema miongoni mwa changamoto wanazokutana nazo ni Pamoja na tozo katika vikundi vya ushirika vya wakulima wa miwa, ubaguzi wakati wa kuvuniwa mazao yao kutoka shambani na kuchukuliwa kiasi fulani cha miwa kuingizwa kiwandani na kingine kutupwa.

Changamoto nyingine walizozitaja ni kukosekana kwa uwazi wa thamani ya miwa ambayo ndio hutengeneza malipo ya mkulima sambamba na kupewa kazi ya kupeleka miwa kiwandani kwa watu wasio na sifa stahiki.

Kufuatia changamoto hizo zilizotolewa na wakulima hao, Mkuu wa Mkoa Martine Shigela amewataka viongozi wanaohusika akiwemo Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Morogoro Keneth Shemdoe Pamoja na Meneja wa huduma kwa wakulima kutoka kiwanda cha Sukari Kilombero Job Zahoro kutafuta suluhisho la haraka la malalamiko hayo.

Awali akitoa ufafanuzi katika baadhi ya changamoto zilizotajwa na wakulima hao, Meneja huduma kwa wakulima Kiwanda cha Sukari Kilombero Job Zahoro amesema kiwanda kitanzingatia vigezo stahiki katika kuwapata wakandarasi watakaojihusisha na shughuli za ubebaji wa miwa kupeleka kiwandani ili kuondoa changamoto zilizojitokeza.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Hanji Godigodi amewaomba viongozi wa vyama vya ushirika Pamoja na Mrajisi wa Kanda kufuata kanuni na sheria sambamba na kumuogopa Mungu wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ili kulinda maslahi ya wakulima akibainisha kwamba kazi ya Kilimo ni ngumu.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Alhaji Majid Mwanga ameahidi kuwashughulikia viongozi watakaozembea kutatua changamoto zinazowakabili wakulima kupitia vyama vya ushirika vya wakulima wa miwa.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.