• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mmoja afariki dunia 85 wajeruhiwa, RC Shigela awapa pole.

Posted on: July 23rd, 2021

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 85 kujeruhiwa baada ya roli ya kampuni ya Yapi markez inayojenga reli ya kisasa SGR kuigonga treni ya abiria ya reli ya kati iliyokuwa safarini kutoka Kigoma kuelekea Jijini Dar es salaam.

Hayo yamebainishwa Julai 22, Mwaka huu na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro Fortunatus Muslimu alipofika eneo la ajali lililopo kidete Wilaya ya  Kilosa Mkoani Morogoro ambapo amesema ajali hiyo ilitokea katika makutano ya reli na barabara inayotumika kupitisha vifaa vya ujenzi wa reli ya kisasa.

Muslimu amemtaja aliyefariki katika ajali hiyo kuwa ni Dereva wa roli ambaye pia ni mfanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania aliyefahamika kwa jina la Jerald Marandu aliyeigonga treni  hiyo  na kupelekea mabehewa mawili ya treni kuhama njia yake.

‘’…Treni hii ilikuwa inatoka kigoma kwenda Dar es salaam baada ya kufika katika eneo hili ajali ilitokea ambapo roli iliigongo treni, kutokana na kuanguka jumla ya abiria 85 wamejeruhiwa na mmoja amefariki ambaye ni dereva wa roli…’’ amesema Muslimu.

Aidha, Muslim ametoa wito kwa madereva kuchukua tahadhali katika maeneo ambayo  ujenzi wa reli ya kisasa  unaendelea ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika na kuleta madhara katika ujenzi ikiwa ni pamoja na kusimama kwa ujenzi wa barabara na kazi nyingine.

Awali akiwasilisha salamu za pole kutoka kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amewasilisha pole za Rais kwa familia ya wafiwa, abiria wote waliokuwa wakisafiri, Kampuni ya Yepi markez, Shirika la Reli Tanzania -TRC na watanzania wote kwa jumla.

Sambamba na hayo, Shigela ametoa shukrani kwa Kampuni ya Yepimarkez kwa jitihada walizozifanya za kusaidia kuleta mabasi kwa ajili ya kubeba majeruhi na kuwafikisha katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa kwa ajili ya kupatiwa huduma ya kwanza, lakini pia kulinda mali za abiria kutopotea.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro baada ya kutembelea eneo la ajali alifika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa ambapo majeruhi wa ajali hiyo walikuwa wamepelekwa  kupata matibabu ya awali na kuwajulia hali huku akiagiza jeshi la polisi kulinda mizigo yote ya wahanga wa ajali hiyo na kisha kuwafikishia ikiwa salama.


Naye Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa TRC Amina Lumuli amesema kazi zinazoendelea sasa ni kuyafanyia uchunguzi mabehewa 12 kati ya 14 ya treni hiyo kama yako salama kuweza kuendelea na safari, kurekebisha njia ndogo ambayo imepata hitirafu na kunyanyua mabehewa mawili yaliyoanguka pamoja na kichwa cha treni.


Treni hiyo iliyokuwa inatoka Kigoma kwenda Dar es Salam ilikuwa na mabehewa 14 na zaidi ya abiria 1000, kati ya majeruhi hao 85, majeruhi 70 ni watu wazima na 15 ni watoto.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.