• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MOROGORO KUENDELEZA MAPINDUZI YA KILIMO

Posted on: November 2nd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Ali Malima amesema kuwa Morogoro imejipanga kuendelea kuwa kinara katika shughuli za kilimo hususan zao la mpunga ambapo huchangia kwa kiasi kikubwa katika biashara, viwanda na shughuli za kijamii ili kukuza uchumi wa Mkoa na Taifa.


Mhe. Malima ametoa kauli hiyo Novemba 2, 2023 katika mkutano wa msemaji mkuu wa serikali na waandishi wa Habari uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.ukiwa na lengo la kutangaza mafanikio ya serikali ya awamu ya sita ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Mkoani humo.


 Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa dhamira ya kilimo Mkoani humo ni kuongeza  tija ya uzalishaji kutoka tani laki 9 hadi tani Mil. 1.5 za mpunga ili kujiweka katika mazingira mazuri ya usalama wa chakula kwa watu mil 3.2 kwa mujibu wa sensa ya watu na Makazi ya mwaka 2022 waliopo Mkoani humo, hivyo wananchi wanatakiwa kujikita katika shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo biashara, viwanda na shughuli za kijamii.


“…Mkoa wa Morogoro ndiyo namba moja katika uzalishaji wa mpunga ambapo sasa hivi tumefikia uzalishaji wa tani laki 9 na malengo yetu kufikia tani milioni 1.5 kwa mwaka…”amesema Mhe. Adam Malima


Sambamba na hilo, Mhe. Adam amebainisha kuwa wananchi wanapaswa kujua miradi muhimu inayotekelezwa katika maeneo yao na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuzingatia uwekezaji wa sekta za umma na sekta binafsi ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa Mkoa huo.


Katika hatua nyingine, Mhe. Malima amemshukuru Mhe. Rais kwa kuuheshimisha Mkoa wa Morogoro kuwa Mkoa wa Kimkakati ambapo miradi ya kimkakati ikiwemo Barabara kuu na reli ya kisasa ya umeme zinazounga Mkoa wa Kibiashara (Dar es Salaam) na Mkoa wa Makao Makuu ya serikali (Dodoma) hivyo, kutasaidia kukuza uzalishaji wa kilimo, Viwanda na shughuli za kibiashara sambamba na kuongeza pato la Taifa.


Kwa upande wake, Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Mobhare Matinyi amesema kuwa Mhe. Rais amewafikia wananchi katika hatua mbalimbali ikiwemo kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo hususan Barabara ambayo ndiyo chachu ya maendeleo katika sekta zilizopo Mikoani na Nchi kwa ujumla, na kuwataka wakurugenzi kufuata maelekezo ya serikali ili kuendana na kasi ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Bi. Joanfaith Kataraia amesema serikali ya awamu ya sita kwa kipindi cha miaka miwili imetoa zaidi ya Tsh. Bil. 64 katika kutekeleza miradi ya maendeleo ya Halmashauri hiyo ikiwemo sekta ya afya, elimu na utawala ambapo hapo awali wananchi walilazimika kutembea umbali wa kilometa 200 kufuata huduma hizo, hivyo serikali imetatua mahitaji muhimu ya wananchi wa Halmashauri hiyo.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.