• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

Posted on: March 24th, 2021

Uongzi wa Serikali ya Mkoa wa Morogoro umesema utaendelea kukomesha migogoro ya Ardhi, pamoja na mapigano baina ya wakulima na wafugaji ndani ya Mkoa huo kwa lengo la kumuenzi alieyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyefariki dunia Machi 17 mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare wakati wa Kongamano maalum la kuomboleza kifo cha hayati Dkt. John Pombe Magufuli  lililofanyika Machi 23 mwaka huu  katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mvomero na kuhusisha wananchi na viongozi mbalimbali wa dini na Serikali.

Loata Sanare amesema moja ya kazi kubwa aliyokuwa amepewa na hayati Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa uteuzi wake ni kumaliza migogoro kati ya wakulima na wafugaji iliyokuwa ikiendelea Mkoani humo hususan katika Wilaya za Mvomero na Kilosa.

“Nashukuru mungu tulipokutana ametoa pongezi za kutosha kwangu na kwa viongozi wote wa Mkoa wa Morogoro kwamba angalau kwa mwaka mmoja tu tumeweza kudhibiti na kuhakikisha hawawezi kupata taarifa kubwa ya migogoro, kazi hii sikufanya mimi, Mkuu wa Wilaya, wamefanya viongozi wetu wenyeviti na watendaji wa vijiji” alisema Sanare.

Loata Sanere amesisitiza kuwa ili kumuenzi hayati Dkt. John Pombe Magufuli, Mkoa wa Morogoro hauna budi  kusimamia kwa nguvu zote Ulinzi wa watu na mali zao katika Mkoa huo pamoja na amani iliyopo kwa Serikali kushirikiana na wananchi pamoja na wadau mbalimbali ndani ya Mkoa huo.

Akihitimisha hotuba yake, Loata Sanare amesema pamoja na kuendelea kudhibiti migogoro ya wakulima na wafugaji, Dkt. John Pombe Magufuli ataenziwa kwa kuendeleza ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kumbukumbu ya Sokoine inayojengwa Wilayani Mvomero ambapo tayari kabla ya umauti kumkuta alishatoa shilingi 4 Bil. Kati ya shilingi Bil. 12 zinazohitajika kukamilisha ujezi huo, kisha utajengwa mnara au sanamu ya hayati Waziri Mkuu Moringe Sokoine aliyefariki eneo hilo kwa ajali ya gari.

Wakitoa salamu za maombolezo wawakilishi wa wananchi Wilayani Mvomero akiwemo Mwenyekiti wa waendesha Pikipiki – Bodaboda  Ndg. Rashid Mohamed, amesema  hayati Dkt. John Pombe aliwasaidia bodaboda hao kutambua sheria za barabarani na kuwapatia fedha za mkopo kwa riba nafuu ambayo iliwasaidia kujikimu kimaisha na familia zao.

Naye, Katibu wa wafugaji katika Mkoa wa Morogoro Joshua Lugaso amesema kuwa hayati Dkt. John Pombe Magufuli amewasaidia sana wafugaji kwa kuwapatia masoko ambapo viwanda vya nyama zaidi ya vitatu vimejengwa kikiwemo kiwanda cha Longido ambacho kina uwezo wa kuchinja mbuzi 1000 na Ng’ombe 500 kwa siku.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Albinus Mgonya amebainisha baadhi ya mambo ambayo watamkumbuka shujaa huyo kwa kuchapakazi, kuwa wazalendo kwa nchi yao, kupinga rushwa, kupenda maendeleo na kupenda haki pamoja na mabadiliko  chaya kwa manufaa ya jamii.

Sambamba na hayo, Mgonya ametoa wito kwa wananchi wa Mvomero kuenzi mambo yote mazuri aliyoyafanya hayati Dkt. John Pombe Magufuli, ikiwa ni pamoja na kuepuka viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika jamii, kufanya kazi kwa bidii, kutoa huduma bila upendeleo na kutii maagizo ya Serikali.

MWIISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.