• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MOROGORO KUWA KITOVU CHA UTALII WA NDANI.

Posted on: April 3rd, 2025


Mkoa wa Morogoro umetajwa kuwa kitovu cha Utalii wa ndani hapa nchini kwa siku za karibuni  kutokana na urahisi wa kufikika kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania baada ya Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya miundombinu.

Hayo yamebainishwa Aprili 3, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima Ofisini kwake wakati anaongea na Wajumbe wa Chama cha Maafisa Mawasiliano wa Serikali (TAGCO) waliofika kujitambulisha Ofisini kwake na kumweleza kuwa watakuwa na  kikao kazi ndani ya Mkoa huo.

Amesema, uwekezaji Mkubwa uliofanywa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye sekta ya miundombinu hususan ujenzi wa Reli ya mwendo kasi - SGR  umeleta chachu na kufanya Mkoa huo kufikika kiurahisi na hivyo kurahisisha pia sekta ya Utalii na kuwafanya watalii kushawishika kuja mkoani humo kwa ajili ya kutalii.

"Mkoa wa Morogoro sasa hivi ndio mwelekeo mkubwa wa utalii wa ndani Tanzania kwa sababu unafikika kiurahisi kwa uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali wa Treni ya mwendo kasi - SGR" Amebainisha Mhe. Adam Malima.


Pamoja na kuwapokea na kuwakaribisha Mkoani humo, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka Maafisa hao kutumia fursa hiyo baada ya kikao chao kutembelea vituo vya utalii vilivyoko mkoani humo ikiwemo Mbuga ya wanyama ya Mikumi na milima ya Udzungwa ambayo ina vivutio lukuki kama vile maporomoko ya maji, misitu na viumbe hai mbalimbali vya kuvutia.


Sambamba na hayo amewatakia Maafisa Mawasiliano hao mkutano mwema huku akiwataka kujadiliana na kupeana uzoefu ili kuboresha taaluma yao katika kutoa taarifa za Serikali kwa wananchi wake kwa manufaa ya Taifa la Tanzania.


Chama hicho cha TAGCO kitakuwa na Mkutano wake wa kawaida Mkoani humo kwa muda wa siku saba (7) katika hoteli ya Morena iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro mkutano unaotarajiwa kufanyika Aprili 8 - 12, 2025 na ambao utakuwa na washiriki wasiopungua mia tano (500).


MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.