• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro kuwa Mkoa wa kimkakati sekta ya kilimo

Posted on: October 11th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Ali Malima amesema Serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka mikakati Mkoa wa Morogoro kuwa Mkoa wa kilimo biashara ambapo Wilaya ya Gairo itakuwa mfano wa kuigwa katika ajenda ya kukuza kilimo.

Mhe. Malima amesema hayo Oktoba 10, 2023 katika ufunguzi wa maonesho ya kilimo biashara na kilimo marathon yanayofanyika Wilayani Gairo yakiwa na lengo la kukuza kipato cha wananchi sambamba na kukuza mapato ya Halmashauri kupitia sekta ya kilimo.

Mhe. Adam Malima amesema mkakati huo utakaoanzia Wilayani Gairo katika kilimo cha  mazao ya mahindi na alizeti kuongeza tija ya uzalishaji unalenga kuzalisha kutoka gunia tano za mazao hayo kwa ekari hadi gunia 25.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Ada

"...twendeni tukaigeuze Morogoro kama alivyokusudia Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Morogoro ikawe ndio Mkoa wa kimkakati katika uzalishaji wa kilimo Tanzania..." amesema Mhe. Adam Malima

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amemuagiza Katibu Tawala msaidizi sehemu ya uchumi na uzalishaji Dkt. Rozalia Rwegasira kushirikiana na wadau mbalimbali wa Wilayani humo kutoa elimu ya msingi juu ya kilimo biashara kwa wakulima ili kuwa na uzalishaji wenye tija.

Sambamba na hilo Mhe. Malima amewataka Wakurugenzi, Maafisa ugani, Maafisa tarafa, Maafisa watendaji wa kata na vijiji kufahamu masuala ya msingi ya kilimo na kuhakikisha wanawahimiza wakulima kutumia mbegu, mbolea na mbinu za kisasa kwa uzalishaji wenye tija huku wakitunza mazingira ambayo ndio chanzo kikubwa kwenye kilimo.

Mkuu wa Mkoa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa dhamira yake ya kutaka Mkoa huo kuwa wa kimkakati kwani amesema sekta ya kilimo Mkoani humo ina thamani zaidi ya shilingi trilioni 2  kukiongozwa na mazao ya mpunga na miwa.

Kwa upande wake, Katibu Tawala msaidizi sehemu ya uchumi na uzalishaji Mkoani Morogoro Dkt. Rozalia Rwegasira amesema maonesho hayo yatawaelimisha wakulima  namna ya kutumia mbinu bora za kilimo kuanzia matumizi ya mbegu bora, mbolea, viua wadudu na teknolojia za kisasa huku akiwatahadharisha wakulima juu ya uwepo wa mvua za El-nino ambapo amewataka kuandaa mashamba yao mapema ili kuwa tayari kwa kupanda.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema Wilaya hiyo imeanza kutekeleza wa ajenda ya kilimo biashara kwani wakulima zaidi ya 98% hutegemea shughuli za kilimo hata hivyo amesema wakulima hao hawazalishi kwa tija na kwamba maonesho hayo yanaenda kutatua changamoto hizo na kuongeza uzalishaji wenye tija.

Nae, Mbunge wa Jimbo la Gairo Mhe. Ahmed Shabiby ameipongeza serikali ya awamu ya sita kwa kuhakikisha wananchi wa Wilaya hiyo wanapewa umeme na kuomba umeme jazilizi kwa baadhi ya vijiji ambavyo havina umeme kwani amesema  nishati hiyo inasaidia wananchi kutekeleza shughuli zao mbalimbali za kiuchumi ikiwemo shughuli ya kilimo.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.