• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro kuzalisha asilimia 70 ya sukari nchini

Posted on: January 30th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema Mkoa huo kupitia viwanda vyake vya sukari vya Mkulazi, Mtibwa Sugar na Kilombero Sugar utazalisha zaidi ya asilimia 70 ya sukari yote hapa nchini hivyo kupunguza uhaba wa bidhaa hiyo.

Mhe. Malima ameyasema hayo Januari 29, 2024 mbele ya Kamati ya kudumu ya Bunge ya Biashara, Viwanda, Kilimo na Mifugo ambayo imefanya ziara Mkoani humo kujionea hali ya uzalishaji wa sukari pamoja na changamoto zilizopo katika viwanda vya Mkulazi na Mtibwa Sugar.

Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa Mkoa huo utazalisha tani 400,000 kati ya tani 500,000 ambapo kiwanda cha sukari cha Kilombero kitazalisha tani 270,000, Mtibwa Sugar kinatarajia kuongeza uzalishaji na kufikia tani 100,000 kutoka uzalishaji wa sasa wa tani 70,000 na Mkulazi kitazalisha tani 50,000 hivyo amesema hali hiyo itapunguza hivyo uhaba wa sukari hapa nchini.

“…kwahiyo tani 270000 za Kilombero, tani 100000 za Mtibwa 370000 na tani 50000 za Mkulazi zitakuwa tani 420000  kwahiyo sisi Mkoa wa Morogoro tutakuwa tunazalisha asilimia 70 ya sukari inayohitajika…” amebainisha RC Malima.

Aidha, ametaja  mikakati ya mkoa kwa sasa, kuwa ni kuongeza ushiriki wa wakulima wadogo wa zao nilo la miwa ili wachangie uzalishaji wa sukari kwani amesema kwa kufanya hivyo kutainua uchumi wa wakulima wenyewe na taifa kwa ujumla.

Hata hivyo, Mhe. Malima ametaja sababu zinazochangia upungufu wa uzalishaji wa sukari katika viwanda vilivyopo mkoani humo kwa sasa kuwa ni pamoja na mvua zinazoendelea kunyesha huku akiwaomba wadau, Bodi ya Sukari pamoja na Serikali kushirikiana kupata suluhisho hasa kwa kipindi hiki ambacho viwanda vimepunguza uzalishaji.

Naye Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. David Silinde (MB) amempongeza Mkuu wa Mkoa pamoja na watendaji wote kwa kuwa na maono ya kuendeleza sekta ya kilimo cha mazao matano ya kimkakati ambayo ni Karafuu, michikichi, Parachichi, Kakao na Kahawa ambayo yatasaidia kuinua uchumi wa wakazi wa mkoa huo

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Biashara, Viwanda, Kilimo na Mifugo Mhe. Deo Mwanyika ameweka wazi lengo la ziara ya Kamati hiyo Mkoani hapo kuwa ni kujionea sababu zinazopelekea uhaba wa sukari kama ambavyo imeelezwa hivi karibuni na Wizara ya Kilimo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.