• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MOROGORO NA MKAKATI WA KURUDISHA UOTO WA ASILI

Posted on: May 20th, 2022

MOROGORO NA MKAKATI WA KUREJESHA UOTO WA ASILI.

Mkoa wa Morogoro umejipanga upya kuhakikisha unarejesha Uoto wa asili kupitia Mkakati wa kupanda miti katika Mkoa huo kama sehemu ya kuhifadhi, kutunza, kulinda na kudumisha mazingira ya Misitu na uoto wa asili.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akipanda mche wa mti wakati wa Kongamano la wadau wa Mazingira lililofanyika Mei 20 mwaka huu Eneo la Magadu Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela Mei 21 Mwaka huu wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Mazingira lililofanyika kwenye ukumbi wa Magadu Mess uliopo Halmashauri Manispaa ya Morogoro, tukio hilo liliambatana na shughuli ya upandaji wa Miti katika Shule ya msingi ya Magadu kama sehemu ya kutekeleza mkakati huo wa kuhifadhi, kulinda na kutunza Mazingira.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema ni wakati sasa kwa wadau wanaoshughulika na Mazingira kujitathmini na kufanyakazi kwa pamoja kwa kutoa elimu na uwezeshaji wa miche mbalimbali ya miti kwa jamii ili kuhakikisha jamii inawajibika vema katika suala la uhifadhi wa mazingira kwa manufaa ya sasa na ya baadae.





Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Rosalia Rwegasira akipanda mti wakati wa Kongamano hilo.

Aidha, Martine Shigela amesisitiza suala la upandaji miti ili kurejesha hadhi ya Mkoa huo wenye asili ya kuwa na mazingira bora na yenye utulivu kwa binadamu na Wanyama hadi kupelekea uwepo wa mvua nyingi unaosababisha uwepo wa mito mingi inayotiririsha maji yake msimu mzima tofauti na ilivyo sasa.



Mhe. Shigela (wa pili kushoto) akiwa kwenye maandamano na wadau wengine wa mazingira kuelekea eneo la kupanda miti

“Mazingira yetu ndio kila kitu, sote tunakumbukwa kwamba Wasanii waliimba Morogoro maji yanatiririka milimani lakini sasa hivi yanazidi kupungua, sasa lazima kama mkakati wetu ulivyo tuweze kuurudishia hadhi Mkoa wetu wa Morogoro……” amesema Shigela.

“……Kuhakikisha tunahifadhi Uoto wa asili na tunatunza mazingira ili yaweze kututunza na kutusaidia katika Maisha yetu” ameongeza Shigela.

Katika hatua nyingine Martine Shigela ameagiza Wakuu wa Wilaya na viongozi wengine wa Serikali Mkoani humo kuhakikisha kila shule inakuwa na vitalu vya miti na kila mwanafunzi kukabidhiwa mche wa mti wa kupanda kila inapofika mwezi Januari ili kuwa na uhakika wa takwimu zinazotolewa za upandaji miti ziwe na uhalisia.



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akiongea na wadau wa mazingira siku ya Kongamano la Mazingira Mkoani humo Mei 20 mwaka huu

Naye, Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga amebainisha kwamba Kongamano hilo liwe chachu ya kuubadilisha Mkoa wa Morogoro kwa kuonesha uhalisia wa kupanda miti Mkoa mzima ili kudhihirisha kwa vitendo falsafa ya Morogoro ya kijani.



Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga(katikati) naye alishiriki kongamano la wadau wa mazingira

Akiwakilisha Wakuu wa Wilaya wa Mkoa huo, Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabiri Omary Makame ameweka wazi kuwa ni vema kama Mkoa na Taifa, ajenda ya Upandaji wa Miti na Utunzaji wa Mazingira iwe ajenda namba moja kwani utunzaji na uhifadhi wa mazingira ni faida kwa kizazi cha sasa na cha baadae.



Wakuu wa Wilaya za Malinyi, Gairo na Morogoro walikuwepo kwenye Kongamano la wadau wa Mazingira na kutoa michango yao namna ya kuhifadhi Mazingira. kutoka kushoto ni Mathayo Maselle Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Jabiri Omary Makame Mkuu wa Wilaya ya Gairo na Alberty Msando Mkuu wa Wilaya ya Morogoro

Kwa upande wake Bi. Saada Shabibi mdau wa Mazingira Kutoka Rukwa ambaye alishiriki Kongamano hilo ameishauri Serikali kuwa, ili kuhakikisha malengo ya utunzaji na uhifadhi wa Mazingira yanafikiwa kikamilifu ni vema Wizara na idara zote za Serikali kufanya kazi kwa pamoja ikiwemo Wizara ya Nishati kupunguza Tozo ya Gesi ili kudhibiti matumizi ya kuni na Mkaa ambayo huchangia kwa kiasi kikubwa kuharibu Mazingira kwa kukata miti.



Bi. Saada Shabibi (aliyeshika kipaza sauti) akitoa mchango wake wakati wa Kongamano la wadau wa Mazingira.

Aidha Bi. Saada ameishauri Serikali kufanya utafiti wa kupata mbegu za miti zinazokomaa kwa muda mfupi ili kuishawishi jamii kupanda miti hiyo kwa lengo la kuweka uwiano sawa baina ya kasi ya ukataji miti na ukuaji wa miti ili kuziba pengo miti inayokatwa.






Kwenye kongamano hilo pamoja na mada mbalimbali zinazohusu mazingira kutolewa kulienda sambamba na utoaji wa vyeti kwa baadahi ya wadau wa mazingira ishara ya kuwatambua namna wanavyopambana na uhifadhi wa mazingira 


Wadau wa Mazingira Mkoa wa Morogoro wakiwa kwenye kongamano


Mhe. Martine Shigela Mkuu wa Mkoa wa Morogoro (wa tano kulia, waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa mazingira Mkoani humo


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.