• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MOROGORO YAJIANDAA KUWA MJI WA MPIRA.

Posted on: February 16th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema uongozi wa Mkoa huo unajiandaa kuufanya Mji huo kuwa wa kimichezo zaidi hususan mchezo wa Mpira wa miguu kwa lengo la kushawishi timu mbalimbali za ligi kuja Mkoani humo kufanyia michezo yao.

Mhe. Malima ameyasema hayo Februari 15 mwaka huu mbele ya waandishi wa Habari wakati akizungumza na Mtendaji wa Timu ya KMC ya Manispaa ya Kinondoni Bw. Daniel Mwakasungura Ofisini ikiwa Mkoani humo kwa ajili ya kujiandaa na mechi yao dhidi ya timu ya Yanga.

Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha sababu mbalimbali ambazo zimefikiwa kuufanya kuwa Mmkoa wa kimichezo hususan kabumbu kuwa ni Mkoa una vijana wengi wenye vipaji, uwepo wa hali ya hewa nzuri, miundombinu bora ya usafiri kama vile Barabara, Reli ya Kati, Reli ya TAZARA na Reli ya mwendo kasi SGR ambapo zote zinapitia ndani ya Morogoro hivyo wadau wa mchezo kuweza kufika kiurahisi Mkoani humo.

Lakini pia amesema, Morogoro ni mji unaokua kibiashara, uwepo wa vivutio mbalimbali ikiwemo mbuga za Wanyama, maporomoko ya maji na utalii mwingine uliopo katika milima ya Udzungwa ambapo wanamichezo wanaweza kutembelewa mara baada ya kumaliza mechi zao na kujiliwaza hususan kama timu moja haikupata matokeo mazuri.

Hivyo, Mkoa unaendelea kufanya maboresho ya viwanja vyake ili lengo hilo litimie huku wakilenga pia kutaka kutumia vema mashindano ya AFCON yanayotarajiwa kufanyika Afrika ya Mashaariki 2027.

“...sisi hatumo kwenye viwanja vya AFCON vya kuchezea mechi lakini hatuna sababu ya kutokuwemo kwenye viwanja vya kuchezea mechi za kirafiki na kufanyia mazoezi...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Naye Mtendaji wa timu ya KMC Bw. Daniel Mwakasungura kwa niaba ya uongozi na wachezaji wa timu hiyo amemshukuru Mhe. Adam Kighoma Malima kwa kuikubalia timu hiyo kutumia uwanja wa Jamhuri kwa ajili mchezo wao wa mzunguko wa pili dhidi ya timu ya Yanga.

Timu ya KMC inatashuka dimbani Februari 17, 2024 dhidi ya timu ya Yanga katika uwanja wa Jamhuri Mkoani humo, ambapo KMC inatumia uwanja huo kama uwanja wao wa nyumbani.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RAIS MSTAAFU WA AFRIKA KUSINI AWATAKA WAAFRIKA KUENZI MASHUJAA WAO.

    May 23, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.