• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MOROGORO YAJIPANGA KUKOMESHA VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA.

Posted on: March 8th, 2024

MOROGORO YAJIPANGA KUKOMESHA VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA.


Vitendo vya ukatili wa kijinsia vimetajwa kuongezeka kila kukicha Mkoani Morogoro baada ya kuwepo mfululizo wa matukio ya ubakaji kwa wanawake, Watoto na ulawaiti na kupelekea Mkoa huo kujipanga kudhibiti matukio hayo.


Hayo yamebainishwa Machi 7, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima wakati wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa – RCC kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Magadu Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mhe. Malima amesema matukio hayo yameripotiwa kwa kipindi cha Mwezi Februari, 2024 ambapo suala la ubakaji na ulawiti ni miongoni mwa aina ya ukatili ulioripotiwa mara nyingi zaidi huku akibainisha kuwa kwa sasa Mkoa huo umejipanga kuhakikisha matukio hayo yanakomeshwa.


“...ili tuwe mfano kwa Tanzania kwamba hili jambo sisi tumelikasirikia, hatulitaki...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Alex Mukama amethibitisha kuwa matukio ya ulawiti kwa sehemu kubwa yanafanyika shuleni na kwamba jamii imekuwa chanzo cha matukio hayo kutokana na kuziishi baadhi ya mila na desturi zisizofaa.

Naye Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro Mhe. Christina Ishengoma  kwa masikitiko makubwa amesema akinababa kujiingiza kwenye matendo ya ukatili ni jambo baya na ni dhambi kwa mwenyezi Mungu, huku akitaka Elimu zaidi itolewe kwa makundi yote ya akina baba ili kupunguza kasi ya ukatili huo.


Aidha, amewataka wazazi na walimu mashuleni kuchukua nafasi zao kama walezi namba moja katika kufuatilia nyendo vijana/watoto wao na kutaka suala la ukatili liwe ni agenda ya kudumu kwa vikao vyote vya kisheria vinavyofanyika.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Rebecca Nsemwa amesema ucheleweshaji wa utoaji maamuzi kwa kesi za matukio ya Ukatili kwa baadhi ya taasisi za kutoa haki, kwa sehemu kubwa  kunachangia kesi nyingi kutofikishwa Mahakamani na wananchi kuamua kumaliza kesi hizo ngazi ya familia.


Wajumbe wa kikao hicho cha Ushauri kwa Pamoja wamepitisha jumla ya Tsh. 484.054.323,572.61 ikiwa ni Bajeti ya Mkoa huo ya mwaka wa fedha 2024/2025 fedha hizo ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na pia kwa ajili ya miradi ya Maendeleo.


Kati ya fedha hizo, fedha za ndani kwa ajili ya miradi ya maendeleo ni shilingi 60,340,807,578.00 na fedha za nje ni shilingi 42,853,582,056.00


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.