• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro yajipanga kuzalisha mazao ya kimkakati.

Posted on: August 1st, 2023

Mkuu wa Morogoro Mhe. Adam Malima amesema Mkoa kupitia sekta ya kilimo umejipanga kufufua mazao ya kimkakati yakiwemo pamba na kahawa ambayo awali yalikuwa yakizalishwa kwa wingi katika Mkoa huo.

Mhe. Malima ameyasema hayo Julai 31 mwaka huu alipotembelea banda la Halmashauri ya Mvomero ikiwa ni maandalizi ya sherehe wakulima na wafugaji Nanenane alitumia fursa hiyo kukagua vipando na mabanda yaliyopo katika viwanja vya Julius Kambarage Nyerere Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa ajili ya maonesho na sherehe za Nanenane kanda ya mashariki.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema zao la Pamba na Kahawa ni miongoni mwa mazao yenye faida kwa uchumi wa mkulima na taifa kwa ujumla lakini hakuna tija ya uzalishaji wa mazao hayo, hivyo amesema mazao hayo yatawekewa mkazo ili yaendelee kuzalishwa kama awali.

“...kwahiyo hii ni kati ya mazao tunayoenda kuimarisha sana hapa kwetu Morogoro, kahawa kule milimani Mgeta...” amesema Mkuu wa Mkoa.


Aidha, Mhe. Malima amebainisha kuwa miongoni mwa mazao yatayofufuliwa ni pamoja na kahawa ambapo takribani miche milioni moja ya kahawa itatolewa na Taasisi ya utafiti wa zao la kahawa (TaCRI) na kupandwa katika Halmashauri za Mvomero na Morogoro.


Sambamba na hilo, Mkuu wa Mkoa amezitaka Halmashauri kuhamasisha wakulima kulima mazao yenye mchango katika mapato yao, akitolea mfano Halmashauri ya Kilosa imekusanya zaidi ya shilingi milioni 220 kupitia zao la maharage pekee.

Katika ziara hiyo Mhe. Adam Malima aliambatana na Wakuu wa mikoa ya Pwani, Tanga na Dar es Salaam lengo ni kujionea maandalizi ya maonesho ya nanenane ambayo Agosti 1 mwaka huu yatafunguliwa na Mhe. Mizengo Peter Pinda Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.