• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MOROGORO YAJIPANGA UPYA ZOEZI LA ANWANI ZA MAKAZI

Posted on: April 12th, 2022

Viongozi wa Mkoa wa Morogoro wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Martine Shigela wamefanya kikao maalum kwa ajili ya kujipanga upya kumalizia ngwe ya pili ya utekelezaji wa zoezi la anwani za Makazi linaloendelea nchi nzima hivi sasa.

Ikumbukwe kuwa Mkoa wa Morogoro hadi Aprili 12 ndio Mkoa unaoongoza kufanya vizuri katika zoezi la ukusanyaji wa takwimu za anwani za Makazi na kuziweka katika Mfumo wa NAPA na kufikisha asilimia 100.05 ya malengo yake.

Mkoa huo ulijiwekea malengo ya kukusanya takwimu za anwani za Makazi laki sita hata hivyo Pamoja na kuwa halmashauri nyingine hazijakamilisha kazi hiyo bado Mkoa huo mpaka Aprili 12 takwimu zilionekana 618,000 sawa na asilimia 100.05.

Pamoja na mafanikio hayo, Mkuu wa Mkoa huo Martine Shigela ameitisha kikao maalum kwa ajili ya kufanya tathmini ya zoezi hilo na kuweka mikakati madhubuti kwa ajili ya zoezi la uwekaji wa vibao katika Makazi ya watu, taasisi pamoja na vibao elekezi vya Barabara na mitaa.

Martine Shigela pamoja na kuwapongeza viongozi wa Chini yake kwa kufanikisha vema zoezi hilo la ukusanyaji wa takwimuza Anwani za Makazi bado amewataka viongozi hao kuongeza jitihada zaidi kwenye zoezi la uwekaji wa vibao ambalo Kama Mkoa ilikuwa halijaanza kutekelezwa.

Katika kikao hicho ambacho kilihusisha Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri Wajumbe wa Menejimenti ya Mkoa Pamoja na Waratibu wa zoezi la Posti Kodi na anwani za Makazi ngazi ya Wilaya ameelekeza kukamilisha zoezi la uwekaji vibao hivyo kabla au ifikapo Aprili 26 mwaka huu ambapo kila Halmashauri inalazimika kuwa imekamilisha zoezi hilo.

Mkuu wa  Wilaya ya Gairo Jabil Omari Makame kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya wenzake amebainisha sili ya mafanikio ya zoezi hilo kwa Mkoa wa Morogoro kuwa ni Maelekezo mazuri ya Mkuu wa Mkoa Martine Shigela, pamoja na Uratibu mnzuri wa Katibu Tawala wa Mkoa huo Mariam Mtunguja kuwa na timu zinazofuatilia zoezi hilo muda wote na kuwa na ushirikiano mkubwa baina ya viongozi wa juu na wa ngazi nyingine.

Nao waratibu wa zoezi hilo ngazi ya Wilaya akiwemo John Mvanga kutoka Halmashauri ya Mji wa Ifakara ameshukuru namna Uratibu na ushirikiano mzuri ulikuwepo baina ya ngazi ya kitaifa, Mkoa na waratibu wa Halmashauri.

 Amesema, kulikuwa na nafasi na utayari mkubwa kwa ngazi na fursa ya kuuliza swali pale wanapokwama na kusaidiwa. Aidha amebainisha namna wananchi walivyopokea zoezi la anwani za Makazi na kutoa ushirikiano mkubwa kwao.

Mratibu Mvanga amesema uelewa huo kwa wananchi unatokana na uhamasishaji wa kutosha uliokwenda sambamba na utoaji wa Elimu kwao juu ya zoezi hilo hususan faida inayotokana na uwepo wa anwani za Makazi katika jamii.

Kwa sababu hiyo wananchi hata Kama waliendelea kujihusisha na shughuki zao za kawaida ikiwemo kilimo, lakini hawakuondoka kwenda mashambani bila kuacha taarifa zote muhim za zoezi hilo kwa Kiongozi wa mtaa, Kitongoji au kiongozi mwingine wa Serikali suala ambalo anasema liliwarahisishia katika kufanya kazi yao.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.