• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MOROGORO YANG'OA MIZIZI YA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI.

Posted on: February 3rd, 2025



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, amesema Serikali ya Mkoa huo, kwa kushirikiana na vyombo vya kisheria, imefanikiwa kutatua migogoro lukuki ya wananchi, hususan ya wakulima na wafugaji, ambayo hapo awali ilikuwa changamoto kubwa katika Mkoa huo.

Mkuu wa Mkoa Malima amesema hayo wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Kisheria Duniani Februari 3, 2025 ambapo kwa ngazi ya Mkoa, maadhimisho hayo yamefanyika katika Kituo Jumuishi cha Utoaji wa Haki Kanda ya Morogoro, kilichopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Akifafanua zaidi, Mhe. Malima amesema kuwa vyombo vya sheria, hususan Mahakama na taasisi nyingine vimefanya kazi kubwa ya kutenda haki kwa usawa, jambo ambalo limechangia kwa kiasi kikubwa kupungua kwa migogoro hiyo.

"Morogoro imepunguza kwa kiasi kikubwa migogoro ya wakulima na wafugaji. Awali, Mkoa huu ulitambulika kwa wingi wa migogoro hiyo, lakini sasa hatuna tena," alisema Mhe. Malima.

Aidha, amevitaka vyombo vinavyosimamia haki na usawa kuendelea kushirikiana na Serikali ili kutatua migogoro mingine iliyopo, kwa kufanya hivyo wananchi wataweza kuendelea kujishughulisha na shughuli za kiuchumi kwa manufaa yao binafsi na ya Taifa nzima.

Kwa upande wake, Wakili wa Serikali Mkoa wa Morogoro, Bi. Lightness Tarimo, kwa niaba ya Wakili Mfawidhi wa Ofisi ya Wakili ya Mkoa wa Morogoro, ameiomba Tume ya Kurekebisha Sheria ya Tanzania kufanya utafiti wa kina kabla ya sheria kutungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani hatua hiyo ni muhimu ili kuhakikisha sheria zinakwenda sambamba na maendeleo ya sayansi na teknolojia, kama inavyolengwa katika Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050.


Naye, Kaimu Jaji wa Mahakama Kuu ya Morogoro, Bw. Stephen Magoiga, amewasisitiza watumishi wa taasisi za kusimamia haki wanapaswa kufanya kazi kwa uaminifu na kwa weledi wa hali ya juu kwani kukiuka misingi ya uadilifu kunaweza kuongeza migogoro na kuiletea madhara makubwa jamii.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.