• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MOROGORO YAPANIA KUINUA KILIMO CHA VIUNGO

Posted on: January 25th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa amesema Serikali ya Mkoa wa Morogoro imeweka nguvu kubwa katika kuinua sekta ya kilimo hususani kilimo cha viungo kama vile hiriki, karafuu na mdalasini lengo ni kuinua uchumi wa wakulima katika Mkoa huo.

Mhe. Fatma Mwassa ameyasema hayo Januari 24 mwaka huu wakati akipokea miche 10,000 ya karafuu iliyofanyika katika Ofisi za Sustainable Agriculture Tanzania (SAT) zilizopo katika Manispaa ya Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema asilimia 85 ya wakazi katika Mkoa huo ni wakulima ambapo wengi wanalima mazao ya chakula lakini hali zao kiuchumi sio nzuri hivyo wao kama Serikali wanajaribu kubuni kilimo ambacho kitapandisha thamani ya maisha yao kwa kuwaongezea kipato.

“...sasa viungo ni miongoni mwa mazao ambayo yanathamani kubwa ukilima hata kama ni kidogo utauza kwa fedha nyingi kwa hiyo tunataka walime sana viungo ili wawe na kipato kikubwa, lengo letu ni kutengeneza wakulima matajiri”. Amesema Mhe. Fatma Mwassa.

Ameongeza kuwa Serikali ina mpango wa kushawishi kuongeza maeneo mengine kwa ajili ya kuzalisha mazao hayo katika Wilaya za kilombero na ulanga lakini pamoja na faida hizo lengo ni kutunza mazingira katika maeneo hayo.

Sambamba na hilo Mhe. Fatma Mwassa ameomba kupatiwa ushirikiano kutoka kwa taasisi hiyo katika kufanya utafiti wa udongo na hali ya mvua katika Wilaya hizo ili kubaini kama zao la karafuu litaweza kustawi katika maeneo hayo hivyo kuongeza maeneo ambayo zao hilo linazalishwa katika Mkoa huo pamoja na hayo ameipongeza Kampuni ya Viridium kwa kuleta mashine za kuchakata mazao ya viungo kama vile karafuu, tangawizi na hiriki katika Mkoa huo, hivyo kupitia mashine hizo uzalishaji wenye tija utaongezeka Kwa sababu wananchi wengi watahamasika.

Nae Meneja wa kiwanda cha Viridium Tanzania LTD Bwana George Ferreira ambacho kinajihusisha na ukaushaji wa mazao ya viungo kama hiriki na karafuu amesema kiwanda hicho cha kwanza Afrika kina uwezo wa kukausha tani 800 za hiriki kwa mwaka lakini changamoto kubwa ni upatikanaji wa bidhaa hizo za hiriki na uwekezaji walioufanya kwenye kiwanda hicho cha kisasa barani Afrika  unagharimu kiasi cha shilingi billion 2, pia amesema wameongeza mashine za kukaushia karafuu ambapo mwishoni mwa wiki hii watakamilisha ufungaji wa mashine hizo katika kiwanda hicho.

Aidha, Meneja Ferreira amesema kuanzia Disemba 16 mwaka 2022 hadi sasa wamenunua tani 100,010 za karafuu kutoka kwa wakulima zenye thamani ya bilioni 1,000,500,000 pamoja na hayo wanatarajia kujenga kiwanda kipya cha kukausha karafuu na kusema kuwa mwishoni mwa mwaka huu ujenzi huo unatarajia kuanza.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Kilimo endelevu Bi. Janet Maro ameishukuru Serikali kupitia Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na Wakuu wa Wilaya Mkoani humo kwa kuunga mkono juhudi za kuboresha maisha ya wakulima hususani kupitia mazao ya viungo.


Aidha, Bi.Janet amesema kupitia Shirika hilo la kilimo endelevu wameweza kuwafikia wakulima zaidi ya 2,000 katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ambapo takribani miche 200,000 ya karafuu katika Vijiji mbalimbali ndani ya Wilaya hiyo imepandwa, hata hivyo wapo tayari kutoa ushirikiano katika nyanja mbalimbali ikiwemo utoaji wa mafunzo na miche ili kuhamasisha wananchi kujikita katika Kilimo cha mazao hayo pamoja na kuwashirikisha Maofisa Ugani ili waweze kupata uzoefu wa kilimo hicho.

Taasisi hiyo ya kilimo endelevu kwa kushirikiana na kampuni ya Viridiam imetoa miche 10,000 ambayo imegawanywa kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Ulanga, Morogoro Vijijini na Kilombero kwa ajili ya uhamasishaji wa kilimo cha mazao hayo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.