• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MOROGORO YAPOKEA PROGRAM YA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI KWA KUUNGANISHA NA MAZAO YA KIMKAKATI.

Posted on: May 13th, 2024


Uongozi wa Mkoa wa Morogoro umepokea na kuahidi kutekeleza Sera ya Taifa ya Uwezeshaji Kiuchumi ya mwaka 2004 na kwamba itatekeleza program hiyo kwa kuunganisha na program ya Mapinduzi ya Kilimo cha mazao matano ya kimkakati, lengo ni kuinua maisha ya wananchi kiuchumi.

Hayo yamebainishwa Mei 13 na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Ali Malima wakati akifungua kikao cha kutambulisha Program ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi inayojulikana kama Imarisha Uchumi na Mama Samia { IMASA } kilichofanyika Ukumbi wa mikutano wa Ofisi yake.

Amesema, kwa kuwa utekelezaji wa Sera hiyo unategemea shughuli za kiuchumi za Mkoa husika, Mkoa wa Morogoro utajikita kuhamasisha wananchi katika kupanda mazao matano ya kimkakati ambayo ni Karafuu, Kahawa, Kakao, Parachichi na Michikichi ili kutunza mazingira, kupata kipato cha mazao yenyewe na mwisho kuinua Maisha yao kiuchumi.

 

“…sasa mimi nataka sisi ajenda yetu Morogoro iwe improving people’s life …nataka tuichukue hii program ya Morogoro tuitumbukize kwenye IMASA…” Amesema RC Adam Malima.

Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi (NEEC) Bibi Being’i Issa akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kufungua kikao hicho amesema, lengo la Programu hiyo ni kutaka kila mwananchi kutekeleza Sera ya uwezeshaji wananchi Kiuchumi kwa kujihusisha kwenye ujasiliamali na kuondokana na dhana potofu ya kila anayefanya biashara ni mhujumu Uchumi.

“…ukiwa mfanyabiashara ulikuwa unaonekana kama ni mhujumu Uchumi, kwa hiyo sasa hivi tulikuwa tunaiondoa hiyo dhana, kuingiza ujasiliamali na watanzania wafanye biashara kila mtu kwa kazi yake…..” amesema Bibi Being’i.

 

 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa ambaye ndiye msimamizi wa program hiyo, amewataka Watendaji wa Serikali ndani ya Mkoa huo wakiwemo Wakurugenzi wa Halmashauri na Maafisa Maendeleo ya Jamii kutokuwa kikwazo cha utekelezaji wa Programu hiyo,

Aidha, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mali Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Elizabeth Mshote amesema maeneo kama Utalii, misitu, madini, nyuki, Sanaa na usafirishaji ni maeneo yanayoakisi Mkoa wa Morogoro yasiachwe kwenye program hiyo.

Wajumbe wa kikao hicho cha kutambulisha program ya uwezeshaji wananchi Kiuchumi wamekubalina kuwa KILIMO na KUONGEZA THAMANI YA MAZAO YA KILIMO liwe ndilo eneo litakalohusika kuwawezesha wananchi kiuchumi hususan wanawake, Vijana na watu wenye Ulemavu.


 

MWISHO 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.