• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro yapokea Vifaa tiba vya thamani ya milioni 759. RC Malima aishukuru Serikali

Posted on: January 18th, 2024

Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa mikoa ambayo imepata vifaa tiba na dawa vyenye thamani ya shikingi milioni 759 kutoka Wizara ya Afya kupitia Bohari Kuu ya Dawa (MSD), lengo likiwa ni kupunguza vifo vya mama na mtoto pamoja na kuimarisha upatikanaji wa huduma za Afya Mkoani Morogoro.

Akizungumza Januari 17 mwaka huu wakati akipokea vifaa tiba hivyo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita Chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kujali wananchi wake hususan wa Mkoa huo kwani amesema hadi sasa Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa lengo la kuboresha huduma za Afya.

Aidha, Mhe. Malima amebainisha kuwa Mkoa huo umepokea vifaa tiba ambavyo vitasambazwa kwa kila Halmshauri za Mkoa huo ambapo vitagawanywa kwenye zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali huku akisema kuwa vifaa hivyo vitaboresha mara dufu hali ya huduma za Afya kwa wananchi wa Mkoa huo.

“...kwenye Sekta ya Afya tumefanya uwekezaji mkubwa...tunaishukuru sana Serikali na tunamshukuru sana Mhe. Rais...tumemaliza suala la miundombinu kwa kiasi kikubwa sana tunajielekeza kwenye kuboresha kiwango cha ubora wa huduma za afya...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Kwa upande wake Meneja wa Bohari Kuu ya Dawa Tanzania (MSD) Kanda ya Mashariki Bi. Betia Kaema amesema Serikali imeendelea kununua dawa na vifaa tiba kwa lengo la kuboresha huduma za afya hapa nchini ambapo imenunua vifaa tiba na dawa vyenye thamani ya shilingi bilioni 14.7 ambavyo vitagawanywa nchin nzima.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Morogoro utapatiwa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 759 ambapo kila jimbo litapatiwa vifaa tiba vya shilingi milioni 69 huku na kuongeza kuwa usambazaji huo wa vifaa tiba ni wa awamu ya kwanza vifaa tiba hivyo vitasaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Baadhi ya vifaa tiba vilipokelewa Mkoani Morogoro ni pamoja na Vitanda vya wagonjwa 330, vitanda vya kujifungulia mama wajawazito 220, mashuka 1320, magodoro 330 na meza 220 vifaa ambavyo  mwakilishi wa Katibu wa Chama cha Mapinduzi - CCM Mkoa wa Morogoro Ndg. Issack Kalleya amewataka Wakuu wa Wilaya kuhakikisha kuwa vifaa hivyo vinakuwa salama na kutumika kama ilivyokusudiwa.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.