• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro yatoa msaada kwa waathirika wa mafuriko Hanang.

Posted on: December 8th, 2023

Wadau wa maendeleo Mkoani Morogoro wameungana na watanzania wengine kutoa misaada kwa waathirika wa maporomoko ya ardhi katika Mji mdogo wa Katesh Wilaya ya Hanang Mkoani Manyara.

Hayo yamebainishwa leo Disemba 8, 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima wakati akipokea msaada wa mkaa mweupe na majiko kutoka Kampuni ya Viridium Tanzania Limited inayozalisha bidhaa hiyo.

Baadhi ya majiko yatakayopelekwa Wilayani Hanang.

Akizungumza wakati akipokea msaada huo wenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 15, Mhe. Adam Malima amesema msaada unaopelekwa Hanang ni tani 10 za mkaa mweupe, majiko 50 na masufuria 500 kwa ajili ya kupikia huku akisema kuwa msaada huo ni wa awamu ya kwanza, msaada wa awamu ya pili kwa wahanga hao ukitarajiwa kupelekwa wiki ijayo.

Huu ni mkaa mweupe ukiwa kwenye mifuko tayari kwa kusafirishwa kwenda Hanang.

"...sisi Morogoro tunapeleka msaada kwa awamu mbili awamu ya kwanza tuna wawahishia mkaa tani 10 na majiko 50..." Amesema Mkuu wa Mkoa.

Sambamba na hilo Mkuu huyo wa Mkoa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuongoza jitihada za kuwapatia msaada wananchi wa Katesh walioathirika na maporomoko hayo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akipokea Mkaa mweupe na majiko kutoka kwa Afisa Masoko wa Kampuni ya Viridium Tanzania Ltd Bw. Aristotle Nikas kwa ajili ya kupelekwa Hanang.

Kwa upande wake Afisa Masoko wa Kampuni ya Viridium Tanzania Limited Aristote Nikitas amesema wameamua kutoa mkaa huo mweupe tani 10 na majiko 50 ili kurahisisha upatikanaji wa chakula, pia amesema mkaa huo unahamasisha suala nzima la utunzaji wa mazingira.

Naye Katibu wa Chama Cha Mapinduzi – CCM Mkoa wa Morogoro Ndugu Solomon Kasaba amesema chama kinaungana na watanzania wengine kutoa pole kwa waathirika wa maporomoko hayo ya Ardhi yaliyotokea Wilayani Hanang Mkoa Manyara, huku akipongeza juhudi za Serikali kwa kuendelea kutoa misaada kwa waathirika hao.

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi ngazi ya Mkoa wanaendelea na jitihada za kutafuta misaada mingine kwa ajili ya wahanga hao wa maporomoko ya Ardhi kama ambavyo wameshirikiana kupata msaada wa majiko na mkaa mweupe.

Maporomoko hayo hadi sasa yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 70 huku watu zaidi ya 100 wakijeruhiwa.

 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.