• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro yazindua Ushoroba wa kilombero

Posted on: September 5th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mathayo Maselle ameitaka  Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania - TAWIRI wakishirikiana na Shirika lisilo la kiserikali  la STEP kufunga vifaa vya kisasa kwa wanyamapori Tembo ili kufuatilia mienendo ya wanyama hao mahali walipo kwa lengo la kutambua maeneo wanayopitia (shoroba)  na kurahisisha kufanyika kwa mchakato wa matumizi bora ya Ardhi katika maeneo hayo.

Mathayo Masele ametoa rai hiyo Septemba 3 mwaka huu wakati wa kikao cha  uzinduzi wa kamati ya usimamizi wa Ushoroba wa Kilombero wenye urefu wa Km 10 unaounganisha hifadhi ya Udzungwa na Hifadhi ya Mwalimu Nyerere kilichofanyika katika Hoteli ya Udzungwa Twiga iliyopo katika Wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro.

Akiwa Mgeni rasmi katika uzinduzi huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela, Maselle amesema, uwepo wa mitambo hiyo ya kisasa kutambua wanyama wakiwemo Tembo itasaidia kubaini njia wanazopita kwenye makazi ya watu hivyo kuondoa migogoro baina ya Maafisa wa wanyama pori na wananchi wa maeneo yanayopitiwa na shoroba hizo.

‘’Nimefurahishwa na uwepo wa Mkurugenzi Mkuu wa Matumizi Bora ya Ardhi hapa nchini kwani moja ya njia ya kupunguza Adha ya wanyama pori kuingiliana na makazi ya watu ni kufanyika kwa  zoezi ambalo ni shirikishi la matumizi bora ya Ardhi yaani kutenga maeneo ya ushoroba’’ amesema Mathayo Maselle.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya amebainisha baadhi ya majukumu ya kamati ya ushoroba huo kuwa ni pamoja na kusimamia na kurejesha ushoroba, kuhakikisha shughuli za mradi huo zinafanyika kwa ufanisi, kutafuta rasilimali za kuwezesha zoezi hilo linakuwa endelevu pamoja na kusimamia utekelezaji wa miongozo na kanuni za zoezi hilo.

Katika hatua nyingine Mathayo Maselle ametoa wito kwa kamati hiyo kuendelea kuelimisha jamii ili kutambua juhudi za Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan katika kuwaondolea wananchi changamoto ya muingiliano baina ya  Makazi ya watu na wanyamapori  wanapopita katika ushoroba husika.

Naye Afisa Maliasili Mkoa wa Morogro Bw. Joseph Chuwa, amesema, kwa mujibu wa tathmini zilizotolewa hivi karibuni zinaonesha kuwa kuna mapito ya wanyama (shoroba) 66 hapa nchini ambapo moja ya mapito hayo ni ushoruba wa Kilombero unaounganisha hifadhi ya Milima ya Udzungwa na hifadhi ya Mwalimu Nyerere kupitia hifadhi ya mazingira asilia ya Magombera.

Amesema ujenzi wa ushoroba huo wa Kilombero utasaidia kupunguza vifo vya watu vinavotokana na kuawa na tembo, kuwafukuza tembo hao kwa urahisi na kuongezeka kwa thamani ya Ardhi na ushoroba  kuwa sehemu ya utalii hivyo kukuza uchumi wa nchi.

Katika hatua nyingine, Chuwa ametoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa serikali katika nia yake ya kuzifungua shoroba hizo  ili kumuondolea mwananchi kero mbalimbali zitokanazo na wanyama pori hususan Tembo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa tume ya ushoroba huo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Bi. Hanji Godigodi amesema kuzinduliwa  kwa shoroba hiyo Wilayani kwake, ikiwa ni ya kwanza hapa nchini, imehamasisha Wilaya yake kutakiwa kufanya kazi hiyo kwa ufanisini ili iwe mfano wa kuigwa kwa Mikoa mingine hapa nchini.

Naye Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mali Dk. Rozaria Rwegasira kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa huo Bi. Mariam Mtunguja amepongeza waratibu wa Shirika lisilo la Kiserikali la mradi wa STEP kwa kuona umuhimu wa kujenga ushoroba katika ukanda wa Kilombelo kwa lengo la kupunguza na kuzuia muingiliano baina ya wanyama na wananchi wa maeneo hayo.

Mkoa wa Morogoro umekuwa Mkoa wa kwanza hapa nchini kati ya Mikoa 26 ya Tanzania Bara kuzindua kamati ya usimamizi wa ushoroba wa Kilombero uliopo Wilayani Kilombero.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.