• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MPANGO KABAMBE WA KUONGEZA UZALISHAJI SEKTA YA KILIMO MKOANI MOROGORO WAJADILIWA

Posted on: March 16th, 2022

Mpango kabambe wa kuongeza uzalishaji katika Kilimo, Ufugaji na Uvuvi wajadiliwa Morogoro

 Mkoa wa Morogoro hivi karibuni umekuwa na kikao kizito cha kuandaa Mpango kabambe wa kuhakikisha  Mkoa huo unaongeza uzalishaji katika Sekta ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi  kupitia kongani ya kilombero lengo ni kuongeza tija kwa wananchi wake na Taifa kwa jumla.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akiwa katika kikao cha SAGCOT Machi 15 mwaka huu.



Mkuu swa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akiwa kwenye majadiliano wakati wa kikao hicho. kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando

Kikao hicho kilichoshirikisha wadau wa Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kutoka Asasi za Kiraia, Binafsi na Sekta ya Umma Mkoani Morogoro kimefanyika Machi 15 mwaka huu katika Hotel ya Morena iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.



Akizungumza  katika kikao hicho kilichoandaliwa na Kongani ya Kilombero  inayoshughulikia Kilimo katika Mikoa ya Nyanda za juu kusini mwa Tanzania - SAGCOT kwa kushirikiana na Ofisi  ya Mkoa wa Morogoro, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro   Martine Shigela ameweka wazi kuwa Ofisi yake iko tayari kushirikiana na wadau mbalimbali katika sekta ya Kilimo ili kuleta tija ya uzalishaji  na kuifanya Morogoro kitovu cha Kilimo, Ufugaji na Uvuvi.




Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mariam Mtunguja akifuatalia kwa karibu mawasilisho yaliyokuwa yakitolewa na wataalam katika kikao cha SAGCOT

Katika kikao hicho wadau hao waliazimia namna ya kutekeleza mpango huo ambapo Sekta ya Umma ikiahidi kuongeza bajeti kwa ajili ya kuimarisha miundombinu vijijini kama vile barabara, nishati ya umeme, usimamizi wa maji na huduma za kijamii ikilenga kuinua uzalishaji katika Kongani ya Kilombero.



Mkurugenzi Mtendaji wa Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania – SAGCOT Geoffrey Kirenga amebainisha kuwa Kongani ya Kilombero ilifunguliwa mwaka 2019 hata hivyo haikuanza kazi rasmi kutokana na changamoto mbalimbali zikiwemo za miundombinu hafifu ambayo sasa Serikali imeahidi kuongeza bajeti kwa ajili ya kuiimarisha.



Mkurugenzi Mtendaji wa SAGCOT Tanzania Geoffrey Kirenga akieleza malengo ya kikao hicho kilichofanyika Hoteli ya Morena Mkoani Morogoro

Wadau hao lutoka Sekta ya Umma, Asasi za Kiraia na Sekta Binafsi kwa pamoja walisaini Hati ya makubaliano ya kutekeleza mpango mkakati huo wa kuongeza uzalishaji katika sekta ya kilimo, Ufugaji na Uvuvi Hati inayojulikana kama Compact Statement.



 

Kwa upande wao Sekta Binafsi imeahidi kuazisha majukwaa kwa ajili ya kupashana taarifa za masoko ya mazao na kuhamasisha wananchi ufugaji na uvuvi wa kisasa, kulinda miundombinu ya barabari, pamoja na kuunganisha wakulima, Wafugaji na wavuvi  wadogo ili kuwa rahisi kwao kufikika katika kupata mafunzo na mikopo ya kibenki.



Nazo Asasi za kiraia zimeahidi kutoa kwa wakulima mafunzo yanayohusu masuala kifedha pamoja na matumizi bora ya viwatilifu ikiwemo mbolea na mbegu bora za mazao pamoja na kuongeza mahusiano ya karibu baina ya wakulima na wanunuzi wakubwa wa mazao na kutowatumia wanunuzi wa kati wa mazao yao.



Akifunga Kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amewaagiza Wakuu wa Wilaya, Maafisa kilimo na wataalamu mbalimbali wa Sekta ya Kilimo kushirikiana na Taasisi za tafiti na wataalamu wa Afya ya udongo kufanya tathmini ya kutambua mazao yanayofaa kulimwa katika maeneo yao ili kuongeza uzalishaji wa mazao hayo.


Aidha, amesema Mkoa wa Morogoro utashirikiana na sekta binafsi na Asasi za kiraia ili kutanua wigo kwa wakulima wadogo, wa kati na wakulima wakubwa ili waweze kuongeza uzalishaji wa mazao mbalimbali ya kilimo, ufugaji na Uvuvi kwa lengo la kukuza kipato chao na kukuza pato la taifa.



Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mariam Mtunguja akiweka saini hati ya makubaliano ya kukuza uzalishaji wa Cluster ya Kilombero wakati wa kikao kilichofanyika Machi, 15 mwaka huu

”Tutatanua wigo Zaidi ili tuongeze farmers(wakulima) wenyewe tuwasikie kwamba wakulima hawa ambao tunawajua na tunawaona wanahangaika tuwalete hapa wasikie hizi knowledge (maarifa) unauwezo wa kutoka tani 40 au 20 kwa hekta moja hadi kufikia tani 60 au 100 kwa hekta moja” amesema Martine Shigela.


Wenyeviti wa Halmashauri za Wilaya walishiriki kikao hicho. hapa ni Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa ametoa wito kwa wanafunzi wanaomaliza vyuo hapa nchini kujiunga na shughuli za kilimo badala ya kusubiri kuajiriwa serikalini au kwenye makampuni mengine wakati wanaweza kuchangamkia fursa katika Sekta ya Kilimo.


Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mali Mkoa wa Morogoro Dkt. Rozalia Rwegasira amesema Mkoa huo umejiwekea mkakati kwa kila Halmashauri kujikita kustawisha zao moja mahusus linalostawi katika Wilaya husika ili kuwa na wepesi wa kupatikana kwa wawekezaji na wanunuzi.


                                                                                                                          

Kwa upande wake  Mtendaji  Mkuu wa ASA Dkt. Sophia Kashenge  mbali na kuipongeza SAGCOT kwa kuandaa kikao hicho amesema Taasisi yake imejipanga kuhakikisha  wanazalisha mbegu  zenye  ubora ili kuleta tija kwenye uzalishaji ndani ya Mkoa huo.


 

Kongani ya Kilombero ni ya Kongani ya tatu kuanzishwa hapa nchini ikitanguliwa na Kongani ya Mbarali iliyopo Mkoani Mbeya na Kongani ya Ihemi ya Mkoani Iringa ambapo zote zinafikisha 70% ya eneo lote la SAGCOT.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.