• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MRAJISI MOROGORO AITAKA GAIRO KUWA MFANO KILIMO CHA MBOGA MBOGA.

Posted on: June 5th, 2024

Mrajisi msaidizi wa Mkoa wa Morogoro Bw. Kenneth Shemdoe amewataka Viongozi wa Kijani Amcos Limited wa Gairo kuwa mfano katika uzalishaji wa mazao ya Bustani yakiwemo mboga mboga na matunda ili kukuza chama hicho pamoja na kukuza maendeleo ya Wilaya ya Gairo.

Bw. Shemdoe amesema hayo Juni 4, 2024 wakati akifunga mafunzo elekezi kwa viongozi wa Bodi ya Chama cha Ushirika cha Mazao ya Bustani (Horticulture ) ya Kijani Amcos Limited yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chama cha Walimu Tanzania Mkoani Morogoro .

"... tunataka muwe chama cha mfano kwa sababu Gairo ndio chimbuko la mboga mboga na matunda ili mtu akija anataka kuona Chama cha Bustani tutawaleta kwenu..." Amesema Kenneth Shemdoe

Sambamba na wito huo Bw. Kenneth amewataka Viongozi hao kukamilisha taratibu za kuanzisha stakabadhi ghalani ambapo Chama hicho kitakuwa na nguvu ya pamoja katika kupanga bei ili kuona tija ya mboga na matunda wanayolima.

Sambamba na hilo, Bw. Shemdoe amesema Chama hicho cha Kijani Amcos Limited kimesajiliwa kisheria hivyo viongozi hao wanatakiwa kuendesha Chama kwa Umoja bila kuweka ubinafsi ambao hubomoa zaidi kwani Viongozi hutakiwa kutanguliza maslahi ya wengi kwa tija ya Chama.

Katika hatua nyingine, Mrajisi huyo wa Mkoa amemshuku Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame kwa kuviunga mkono vyama vya ushirika katika kuona fursa za Kilimo biashara Wilayani humo.

Kwa upande wake, Afisa Ushirika wa Wilaya ya Gairo Bw. Omari Issa amewashukuru wataalamu, wawezeshaji pamoja na wadau mbalimbali waliosaidia kufanikisha mafunzo hayo ambayo yatawaongoza Viongozi katika utendaji wa majukumu ya chama kwa maslahi ya wengi na kuahidi kuendelea kusimamia chama hicho ili kutengeneza uhusiano mzuri wa uzalishaji wa mazao ya Bustani.

Kwa niaba ya wanachama, Mwenyekiti wa Chama cha Kijani Amcos Limited Bw.Gabriel Grasiford Balisidya ameushukuru uongozi wa Ushirika na wawezeshaji kutoa mafunzo yatakayowasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao kwani hapo mwanzo hawakujua namna ya utendaji kazi katika chama hicho.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.