• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Msaada wa huduma ya kisheria kuimarishwa.

Posted on: July 7th, 2021

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Ndugu Amon Mpanju amesema moja ya majukumu ya Wizara hiyo ni kusimamia na kuratibu upatikanaji wa huduma ya Msaada wa Kisheria hapa nchini na jukumu hilo linatokana na dhamira ya Serikali ya awamu ya sita katika kupanua wigo wa upatikanaji wa haki na kuwafikia wananchi wa pembezoni.

Mpanju amebainisha hayo Julai 6 mwaka huu wakati akifungua mafunzo ya Kamati ya Uratibu wa Msaada wa Kisheria Mkoa wa Morogoro yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Flomi Mkoani humo.

Amesema, makundi hayo mara kadhaa yamekuwa yakikosa kupata haki zao jambo ambalo ni takwa la kikatiba kwa sababu tu ya hali zao za kiuchumi na kwamba Serikali lazima iondoe hali hiyo  kwani kutosaidia upatikanaji wa haki kwa makundi hayo ni kutotekeleza Katiba ipasavyo.

“sasa ili kuwe na usawa lazima ubainishe makundi ambayo hayaifikii huduma hiyo kwa hiyo, ukiangalia suala la huduma ya msaada wa kisheria msingi wake, mzizi wake unatokana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977”. Amesema Mpanju.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Ndugu Gliffin Mwakapenje yeye alijielekeza kuihimiza Kamati za Uratibu za Mikoa kutumia sheria ya usuluhishi ya mwaka 2020 ambayo ina mifumo inayoruhusu watu waliokinzana kufikia njia ya maridhiano badala ya kupelekena polisi au mahakamani ili kupunguza gharama kwa wahusika wenyewe na Serikali kwani itapunguza pia idadi ya wafungwa magerezani.

Huku Bi. Grace Makwinya ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Rasilimali Watu katika Wizara hiyo akieleza majukumu ya Kamati za Uratibu za Mikoa kuwa ni pamoja na kutoa huduma ya msaada wa kisheria kwa watoto, makundi maalum na jamii nzima hususan wale waasio na uwezo katika kutafuta haki zao. 

Aidha, Bi Grace amezitaka Kamati hizo kuwa wazi katika utendaji wao wa kazi, kufanya kazi bila upendeleo wala ubaguzi kwa kutumia kigezo chochote kiwe cha hali, jinsia dini au kisiasa.

Nao washiriki wa Kikao hicho wametoa maoni yao namna ya kuimarisha Kamati hizo akiwemo Dkt. Thobias Mnyasenga ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe ambaye ametaka kuwepo umakini katika kufanya maridhiano kwa kuwa makosa mengine hayatakiwi kufanyiwa maridhiano ikiwemo ubakaji badala yake makosa kama hayo lazima kuviachia vyombo vya kisheria.

Naye Bi. Marcelina Kibena ambaye ni Mjumbe wa Kamati hiyo ya Uratibu wa Msaada wa Kisheria ambaye pia ni kiongozi kwenye shirika la Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania – MVIWATA  amesema ili Kamati hiyo iweze kufanya kazi yake inavyotakiwa hususan katika kutatua migogoro, ni vema matamko ya wanasiasa hapa nchini yawe yanaendana na  mabadiliko ya sheria kwa wakati uliopo.

Kamati za Uratibu ngazi ya Mikoa zimeundwa baada ya kuona kuna umuhimu wa uwepo wa Uratibu wa wadau wanaojishughulisha na utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria kwenye mikoa huku lengo lake hasa likiwa ni kuwasaidia wananchi kupata haki zao za kimsingi.

MWISHO


 

 

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.