• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mtu mmoja auawa kwa risasi Kiwanda cha sukari Mkulazi, RC Malima atoa neno.

Posted on: October 17th, 2023

Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Nawabu Yakubu Almasi (36) aliyekuwa mfanyakazi wa ujenzi katika kiwanda cha sukari Mkulazi amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa baada ya kutokea vurugu kati ya Walinzi kutoka Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Magereza (SHIMA) na wafanyakazi wa kiwanda cha sukari Mkulazi kilichopo Mbigiri Wilayani Kilosa, Mkoani Morogoro.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akizungumza na wafanyakazi wa ujenzi katika kiwanda cha sukari Mkulazi.

Tukio hilo limetokea Oktoba 17 majira ya saa 12 asubuhi kwenye mlango wa kuningilia kiwandani hapo wakati wafanyakazi hao wakijiandaa kuingia ndani kuanza kazi.

Hawa ni baadhi ya wafanyakazi wa ujenzi katika kiwanda cha sukari Mkulazi

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amefika kiwandani kwa lengo la kutoa pole Kwa tukio hilo na kusikiliza chanzo cha vurugu hizo zilizopelekea kifo cha mtu mmoja. Akitoa majumuisho ya tukio hilo Mkuu wa Mkoa Adam Malima amethibitisha kutokea kwa vurugu kiwandani hapo na kubainisha kuwa uchunguzi zaidi wa tukio hilo unaendelea.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akiwa na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Wilaya, viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa na Wilaya pamoja na uongozi wa Kiwanda cha sukari Mkulazi wakitoa pole baada ya kutokea kwa tukio la mauaji.

Aidha, amesema Askari waliohusika na tukio hilo kwa sasa wanashikiriwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano zaidi.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Serikali imesikitishwa na tukio lililotokea kiwandani hapi ambalo limepelekea kifo cha mtu mmoja na kuahidi kuwa itasimamia shughuli zote za mazishi.

“...Serikali ya Mkoa inahuzunishwa sana na kifo cha kijana wetu huyu anaitwa Almasi, mimi nimeshaongea na wazazi wake...na Serikali itasimamia mazishi yake kwa kushirikiana na Kampuni ya Mkulazi...kubwa, niseme tu uchunguzi unaendelea...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Hii ni baadhi ya mitambo katika kiwanda cha Sukari Mkulazi

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi wa Mkoa huo kuacha tabia ya kuharibu miundombinu inayojengwa na Serikali Kwa kutumia Fedha nyingi.

Kwa upande wake Mke wa marehem Bi. Shamsa Amir amesema anaamini Serikali itamsaidia kupata haki yake. Ameongeza kuwa mume wake amemuachia watoto wawili wadogo hivyo kifo chake ni pigo kwa familia hiyo.

Bi. Shamsa Amir mke wa marehem Nawabu Almasi

Nao mashuhuda wa tukio hilo akiwemo Bw. Abdul Salim amesema changamoto kubwa ni suala la ulinzi katika kiwanda hicho ambapo walinzi wamekuwa na tabia ya kuwanyanyasa wafanyakazi na kuwatolea maneno makali ikiwemo kuwatukana.

Bw. Abdul Salim shuhuda wa tukio hilo.

Mwili wa marehem umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya uchunguzi zaidi, huku majeruhi wa katika tukio hilo Bw. Said Said amelazwa katika Zahanati ya Kiwanda cha hicho cha sukari na hali yake inaendelea vizuri.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.