• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MUFTI WA TANZANIA AWATAKA WANANCHI KULINDA MAZINGIRA.

Posted on: November 14th, 2022

Mufti wa Tanzania Shekhe Abubakar Zubeir amewataka watanzania kuyalinda mazingira kwa kuwa mazingira ndio uhai wa mwanandamu kwani mazingira ndio chanzo kikubwa cha mvua hapa duniani.

Shekhe Abubakar Zubeir ametoa kauli hiyo Novemba 13 mwaka huu wakati akihutubia waumini wa dini ya kiislam kwenye sherehe ya Mulid ya Mtume Muhammad (S.A.W) iliyofanyika katika ukumbi wa Tanzanite katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.



Mufti wa Tanzania Shekhe Abubakar Zubeir akihutubia wananchi kwenye sherehe ya Maulid ya Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika katika ukumbi wa Tanzanite Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Shekhe Zubeir amesema suala la mazingira limetajwa katika kitabu kitukufu cha Kuraan, ambapo Mwenyezi Mungu amesisitiza utunzaji wa vyanzo vya maji, utunzaji wa misitu na mazingira yote kwa ujumla.

“...Mazingira yametajwa kwenye Kuraan tukufu,tunzeni mazingira, tunzeni vyanzo vya maji... ” amesema Shekhe Abubakar Zubeir.

Aidha, Mufti amesema kumekuwa na tabia za baadhi ya watu kuharibu vyanzo vya maji, kukata miti hovyo, kuchoma misitu hivyo kutokana na shughuli hizo zimesababisha mvua zisiwe za kutosha katika maeneo mengi hapa nchini.




Sambamba na hilo Shekhe Abubakar Zubeir amewataka wananchi kuendelea kuomba na kuacha maovu ili Mwenyezi Mungu aweze kuleta mvua kwa wakati Pamoja na kuleta neema nyingine kwa watanzania wote.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa wakati akitoa salamu za Mkoa, amewataka wakazi wa Mkoa huo kwa Pamoja kutii maagizo yanayotolewa na Viongozi wa Serikali katika ngazi ya Taifa na ngazi nyingine hususan katika suala zima la utunzaji wa mazingira ili kuondokana na uhaba wa mvua unaochangiwa kwa kiasi kikubwa na shughuli za kibinadamu.



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akisikiliza hotuba kutoka kwa mgeni rasmi Shekhe Abubakar Zubeir kwenye sherehe ya Maulid ya Mtume Muhammad (S.A.W).

Fatma Mwassa amesema kuwa uhaba wa mvua na ukame kwa sasa unatokana na shughuli za kibinadam katika vyanzo vya maji zikiwemo shughuli za uchomaji misitu, kuchungia mifugo kwenye vyanzo vya maji, Pamoja na shughuli za ujenzi maeneo ya milimani, hivyo amewataka wananchi Mkoani humo kulinda mazingira ili kupata mvua za kutosha.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wazazi Mkoani humo kuwapa Watoto wao elimu kwa kuwapeleka shule kwa muda mwafaka ili kuwapa haki ya kupata elimu zote mbili ya duniani na elimu ya dini.

Nae Bw. Fikiri Juma Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Morogoro kwa niaba ya waumini wa dini ya kiislamu katika Mkoa huo ameomba kujengewa Msikiti mkubwa na wa kisasa ili kukabiliana na wingi wa watanzania wanaohamia Morogoro kwa kasi.



Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa wageni waliohudhuria sherehe ya Maulid ya Mtume Muhammad (S.A.W), Kushoto ni Mhe. Mathayo Massele Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Mhe. Jabir Makame Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Ngollo Malenya Mkuu wa Wilaya ya Ulanga, Mhe. Albert Msando Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mjini.

Aidha, Mwenyekiti huo amemsifu Mufti wa Tanzania kwa kuwa mtulivu hivyo kufanya BAKWATA kuwa tulivu tangu aliposhika wadhifa huo.

Hafla hiyo ya Maulid imeenda sambamba na dua ya kumuombea Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uongozi wake ili aweze kuiongoza vizuri nchi yetu kwa matakwa ya mwenyezi Mungu.



Mufti wa Tanzania Shekhe Abubakar Zubeir akitoa zawadi za Vitabu vitukufu vya Kuraan kwa Mashekhe wa Wilaya za Mkoa wa Morogoro.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.