• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mwenge wa Uhuru waanza kutimua vumbi Mkoani Morogoro

Posted on: August 5th, 2021

Mwenge wa Uhuru  2021 umeanza kukimbizwa Mkoani Morogoro ambapo leo Agosti 4 umeanza kukimbizwa katika Wilaya ya Kilosa na kufanikiwa kutembelea miradi mitano na kupongeza utekelezaji wake huku ikikataa kuweka jiwe la msingi mradi mmoja.

Akiongea mara baada ya kukamilika kusomwa kwa Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyosomwa na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Ndg. Yohana Kasitila, Kiongozi wa mbio za  Mwenge wa Uhuru Kitaifa LT Josephine Paul Mwambashi amesema Mwenge wa Uhuru haukuweza kuweka jiwe la msingi mradi huo  kutokana na kukosa nyaraka za malipo ya ujenzi wake.

Amesema, mradi huo ambao unagharimu kiasi cha Tsh. 338 Mil. tayari umeshalipa wakandarasi wa mradi huo jumla ya Tsh. 280 lakini hakuna hati zozote za malipo zilizopatikana, hivyo mwenge wa uhuru pamoja na kuwapongeza Viongozi wa Wilaya ya Kilosa kwa kufanya vizuri miradi mingine minne iliyotembelewa na mwenge lakini hautaweka jiwe la msingi katika mradi huo ambao uko katika kituo cha Afya Cha Mikumi.

Aidha, Lt. Josephine Mwambashi ametumia fursa hiyo kutoa angalizo kwa viongozi wanaopewa dhamana ya kusimamia miradi ya maendeleo kuwa wazalendo katika kusimamia miradi hiyo kwa Sababu Serikali inatoa fedha  hizo kwa ajili ya watanzania kupata huduma muhimu zikiwemo za Afya, maji na barabara.

 Wakati wa makabidhiano ya Mwenge huo wa Uhuru yaliyofanyika katika Kijiji cha Ruaha Mbuyuni Wilayani Kilosa, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela alibainisha kuwa Mwenge wa uhuru 2021 ukiwa Mkoani humo utakimbizwa umbali wa km 1,294.45  na kupitia jumla ya miradi 44 yenye Thamani  ya zaidi ya Tsh. 9 Bil.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Majid Mwanga alitoa taarifa kuwa mwenge wa uhuru utapitia miradi ya maendeleo mitano yenye thamani ya zaidi ya Tsh.2.2Bil. ambapo kati yao mradi mmoja atazinduliwa, mmoja utawekewa jiwe la msingi, miwili itaonwa na mmoja utafunguliwa huku akisema kuwa miradi hiyo iko katika sekta ya Afya, Maji na Elimu.

Ameongeza kuwa katika utekelezaji wa miradi yote hiyo Serikali kuu imechangia Tsh.1,348,431,600/=, Halmashauri ya Wilaya ya Kikosa kiasi cha Tsh. 470,993,161 na Tsh. 205,295,000 ni mchango kutoka kwa wananchi.

Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo ukitokea Mkoa wa Iringa ambapo ulikimbizwa kwa siku tatu katika Wilaya zake za Mufindi, Iringa na Kilolo.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.