• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MWENGE WA UHURU WAPIGA HODI MOROGORO

Posted on: August 24th, 2022

Mwenge wa Uhuru waanza kukimbizwa Mkoani Morogoro

Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2022 umeanza kukimbizwa Mkoani Morogoro baada ya kukamilisha kukimbizwa Mkoani Dodoma na kupokelewa Mkoani Morogoro huku ukitarajiwa kupitia miradi ipatayo 50 yenye thamani zaidi ya shilingi 13.5 Bil.

Mwenge huo wa Uhuru umepokelewa leo Agosti 24 ukitokea Mkoani Dodoma na utakimbizwa katika Halmashauri  tisa (9) zilizopo katika Mkoa huo ambazo zina jumla ya umbali wa Km 2048.

Akiongea muda mfupi baada ya kupokea mwenge huo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bi. Fatma Mwassa amesema Mwenge huo utakimbizwa kuanzia Agosti 24 hadi Septemba 01 mwaka huu na Septemba 02 Mwenge huo utakabidhiwa Mkoa wa Iringa.

Akiainisha Miradi itakayopitiwa na Mwenge huo, Bi. Fatma Mwassa amesema  Mwenge huo wa Uhuru wa mwaka huu 2022 wenye kauli mbiu “sense  ni Msingi wa Mipango ya Maendeleo: shitriki kuhesabiwa, tuyafikie  maendeleo ya taifa utapitia miradi ya maendeleo 12 ya sekta ya Elimu, Sekta ya Afya 9, Maji 9, Barabara miradi 7, na Utawala Bora mradi mmoja.

Miradi mingine itakayopitiwa na Mwenge huo ni Maendeleo ya Jamii/Vijana miradi 9, Sekta binafsi miradi 3 na kufanya jumla ya miradi yote kufikia 50 huku lengo la miradi hiyo ikilenga kutekeleza azma ya utekelezaji wa Mkakati wa kukuza Uchumi na kuondoa Umaskini Tanzania (MKUKUTA).

Kwa upande wake Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa mwaka 2022 Sahili Geraruma amezitaka Halmashauri za Mkoa wa Morogoro kulipa mara moja fedha za mfuko wa maendeleo ya vijana wanazodaiwa, kabla ya Mwenge huo wa uhuru haujawasili katika halmashauri zao.

Aidha, Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa ameendeleo kuhimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye zoezi la Sensa ya watu ambalo limeanza Agosti 24 mwaka huu kwa kuwa amesema sense ya watu ndio msingi wa mipango ya maendeleo na zoezi hilo litachukua siku saba kabla ya kufika mwisho tangu lilipoanza jana Agosti 23.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabir Makame katika nyakati tofauti wakati wa kukimbiza mwenge wa uhuru Wilayani kwake, ameaahidi kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa na Mwengewa huo katika kukamilisha miradi ya maendeleo iliyopitiwa ili kuwa bora zaidi.

 

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.