• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mwenge wa Uhuru wapongeza juhudi za wananchi kuchochea maendeleo

Posted on: May 7th, 2023

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 Ndg. Abdallah Shaib Kaim amewapongeza Wananchi wa Kata ya Namgezi iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga kwa kujitolea nguvu zao kuazisha ujenzi wa madarasa matano ya shule Shikizi ya Namgezi iliyopo wiliayani humo.


Ndg. Shaib ametoa pongezi hizo Mei 7 mwaka huu wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa vyumba hivyo vitano vya madarasa ya shule ya msingi Namgezi baada ya mwenge wa Uhuru kuanza kukimbizwa Wilayani humo.


 “tunatambua mchango wenu hakika, hii ni level ya uelewa mkubwa, mmehamasika na kutoa michango yenu ninyi ni wananchi wazalendo wa Tanzania...hongereni, mwenge wa Uhuru unawapenda...” amesema Ndugu Abdallah Shaib.


Kwa upande Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Namgezi Bw. Halifa Mlesa akisoma taarifa ya ujenzi wa madarasa hayo ya shule amesema ujenzi huo unahusisha vyumba vitano vya madarasa, Ofisi moja na matundu 6 ya choo huku akibainisha kuwa hadi sasa ujenzi huo umegharimu shilingi milioni 77 na kwamba shule hiyo itaondoa changamoto ya wanafunzi kutembea umbali wa kilometa 8.


Akiwa katika mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya cha Ruaha Tarafa ya Ruaha Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge ameonekana kuridhishwa na ujenzi wa kituo hicho kwa ubora wa vifaa vilivyotumika, ufundi na matumizi ya fedha za mradi huo (Value for Money) na kutaka kuendeleza uaminifu huo na kuwataka kukamilisha haraka mradi huo ili utoaji wa huduma zake uanze mara moja.


Nae, Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Ruaha, amesema ujenzi wa kituo hicho uliibuliwa na wananchi kuanzia 2019 kwa kuchimba msingi wa jengo la Wagonjwa wa nje (OPD), unaogharimu shilingi milioni 506, ambapo hadi sasa wamepokea zaidi ya shilingi 382 kutoka Halmashauri.


Mwenge huo wa Uhuru umepitia, kuona miradi miwili, kuzindua mradi mmoja, na kuweka mawe ya msingi miradi mitano yote ikiwa na thamani ya shilingi 1.8 Bil.


Mwenge wa uhuru kesho Mei 8 unatarajia kuendelea na mbio zake Wilayani Malinyi Mkoani humo ikiwa ni siku ya tatu tangu Mwenge huo uingie mkoani Morogoro.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.