• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA ULANGA

Posted on: April 24th, 2024

Ni siku ya tano tangu Mwenge wa Uhuru 2024 kukimbizwa Mkoani Morogoro. Licha ya kukumbana na mabonde na milima, tope na kuvuka maji mengi, Mwenge wa Uhuru umefanikiwa kuwasili katika Halmashauri ya Ulanga, Halmashauri ya tano kati ya Halmashauri tisa za Mkoa wa Morogoro.

Ukiwa Wilayani Ulanga Mwenge wa Uhuru umezindua mradi wa Bustani ya Miche ya Mitiki kwa mfumo wa Kitalu nyumba (Green House). Ni mradi wa uhifadhi wa mazingira na unamilikiwa na Kampuni ya KILOMBERO VALLEY TEAK COMPANY (KVTC). Ni kampuni inayojishughulisha na uoteshaji wa miche, upandaji wa miti mashambani na uchakataji wa magogo yatokanayo na miti iliyovunwa.


Meneja wa KVTC Bw. Jeremia Gumadi anasema mti wa mtiki ni mti mgumu ambao unatumika kwa kutengenezea furniture na vyombo vya baharini kwa sababu ni mti mgumu hauozi lakini pili hauzami badala yake unaelea. Lakini pia TEAK unatumika kwa kutengenezea flemu za Milango na madirisha Pamoja na vifaa vya michezo mbalimbali.

Aidha; Bw. Gumandi amesema KVC ina hekta 28,000 kati ya hizo hekta 8,000 zimepandwa miti ya mitiki na eneo la hekta 20,000 limeachwa kwa ajili ya miti ya asili kwa ajili ya kutunza mazingira.


Mradi huu unagharimu kiasi cha shilingi 379,420,000, na unalenga kuzalisha miche 600,000 kila mwaka ambapo miche 400,000 hupandwa katika shamba la KVTC na miche 200,000 hugawiwa kwa wananchi ili wapande kwenye maeneo yao na hivyuo kutunza mazingira.

Manufaa ya mradi huu ni Pamoja na kupunguza athari za mabadiliko ya tabia nchi, kutoa kodi kwa serikali, vijiji 11 vinavyopakana na kampuni ya KVTC vinapata mrahaba Pamoja na kutoa ajira ya wananchi 700 inyowazunguka.


Kabla ya Mwenge wa uhuru 2024 kuzindua mradi huo, ujumbe mwenge ulitolewa kwa wananchi  na msisitizo mkubwa ulikuwa ni kutunza mazingira kama ilivyo kwenye ujumbe wa Mwenge, Tunza mazingira na shiriki uchaguzi wa Serilikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu.


Ukiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga, Mwenge wa Uhuru 2024 utatembelea miradi 8 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi 2.9 Bil. ukitembea na kaulimbiu ya UHIFADHI WA MAZINGIRA NA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA.

Kesho Aprili, 25,2024 mwenge wa uhuru utakimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi.




MWISHO



Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.