• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mwenyekiti wa Kijiji mbaroni kwa kuuza Ardhi..

Posted on: January 13th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare ameagiza Mwenyekiti wa Kijiji cha  Vianzi Elias Chapakazi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kukamatwa mara moja kwa tuhuma ya kuuza Ardhi ya wananchi kinyume na sheria za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Loata ametoa agizo hilo Januari 12 mwaka huu Ofisini kwake mara baada ya kikao cha pamoja kilichomhusisha Mkuu wa Wilaya Mvomero  Albinus Mgonya, Afisa Ardhi, Wenyeviti wa Vijiji, Watendaji wa vijiji na Kata na Wakulima kutoka katika Halmashauri ya hiyo.

Mwenyekiti wa Kijiji cha  Vianzi (kushoto) Elias Chapakazi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero akishikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuuza Ardhi ya wananchi.

Loata Sanare amesema Mwenyekiti wa Kijiji na au Kitongoji haruhusiwi kuuza Ardhi ya eneo lake la utawala bali anaruhusiwa kupokea maombi ya kuuza ardhi na kuyawasilisha katika serikali ya kijiji na Serikali ya kijiji inajadili kisha kupeleka kwenye mkutano mkuu wa kijiji ili ambapo maamuzi ya kukupa au kumnyima mwombaji wa Ardhi hutolewa.

‘’Naombeni fuateni taratibu zote za kisheria, Mwenyekiti wa Kitongoji haruhusiwi kugawa Ardhi, unachoruhusiwa ni kupokea maombi ya wananchi wako wanaotaka Ardhi lakini maombi yanapelekwa kwenye Serikali ya kijiji, serikali ya kijiji inajadili ikiona kuna sehemu ya kupewa inapeleka kwenye Mkutano mkuu wa kijiji, mkutano mkuu wa Kijiji ndiyo wanaopaswa kukupa Ardhi’’ amesisitiza Sanare.

Katika hatua nyingine, Loata Sanare amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Hassan Njama kumbadilishia kituo cha kazi mtendaji wa Kijiji cha Vianzi Magaly Richard na kumpeleka Mtendaji mwingine ambaye atasimamia zoezi la kupokea barua za Malalamiko ya Ardhi alizokuwa anagawa mwenyekiti wa Kijiji cha Vianzi.

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero (wa kwanza  kushoto) Albinus Mgonya akisikiliza maelekezo ya Mkuu wa Mkoa Loata Sanare dhidi ya hatma ya mgogoro wa Ardhi uliopo katika Wilaya yake.

Pia, Mkuu huyo wa Mkoa amesema amebaini  baadhi ya wananchi wa Vijiji vingine vya Halmashauri hiyo wana barua kutoka kwa barozi wa nyumba kumi wa Chama cha Mapinduzi – CCM ambao wamepewa nyaraka za kuuziwa mashamba na balozi wa nyumba hizo jambo ambalo ni kinyume na taratibu zilizowekwa na Serikali.

Kwa uopande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Albinus Mgonya amesema eneo ambalo limehusika sana kuuzwa linamilikiwa na mwekezaji Balozi Namfua ambaye anamiliki hekali 2000 kwa shughuli za kilimo.

Mgonya amesema hekali 2000 ni nyingi kumilikiwa na mtu mmoja hivyo ametuma kamati ambayo inashirikiana na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuunda hoja ya kumuomba mwekezaji wa eneo hilo kubaki na hekali 1200 huku hekali 800 zinazobaki ziweze kutumiwa na wananchi endapo mamlaka husika itaridhia mapendekezo hayo.

Aidha, Mgonya ameelezea kuwa wamefanya tafiti na kubaini uwepo wa kaya 72 zina makazi katika eneo hilo ambazo zinaendeleza shughuli tofauti za kibinadamu kutokana na kupewa eneo hilo kinyume na taratibu ambapo hekali 800 kati ya 2000 tayari zinatumika na wananchi hao.

Naye, afisa Ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Thomas Nhegeji ameeleza mgogoro wa Ardhi ulipo baina ya kijiji cha Kimambila na Wami Luhindo ambao unapelekea vijiji hivyo kushindwa kugawa Ardhi kwa kufuata sheria au wanafuata  sheria lakini wanajikuta wamevuka mipaka ambapo Kijiji kingine kinadai kimeingiliwa kwenye mipaka yake.

Nao wananchi wa vijiji hivyo akiwemo Susu Nestory Susu Mkazi wa Kijiji cha Wamiluhindo, amesema Kiongozi wa Kijiji cha Vianzi alikuwa akiuza maeneo  kiholela na hadi kupelekea kuuza maeneo ya vijiji vingine, hivyo ametoa pongezi kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  kwa uamuzi ambao ameuchukua ili liwe funzo kwa viongozi wengine wa aina hiyo.

Mtendaji wa Kata ya Dakawa Haji Luvanga ametaja sababu kubwa kwa baadhi ya viongozi ngazi ya Kijiji kujihusisha katika kuuza Ardhi kuwa ni kutokana na kutokuwa na uelewa wa utaratibu wa kuuza Ardhi katika maeneo yao, pia viongozi kuwa na  tamaa ya fedha katika kazi zao.

Luvanga ametoa wito kwa Watendaji wa Vijiji kuwa karibu na wananchi ili kubaini viongozi ambao wanauza Ardhi bila kufuata kanuni, sheria taratibu na kanuni zilizowekwa na Serikali.

Naye Elias Chapakazi Mwenyekiti wa Kijiji cha Vianzi ambaye ni mtuhumiwa wa kosa la kuuza Ardhi ya Kijiji amekanusha madai ya yanayomkabili ya kuuza Ardhi hiyo  na kwamba hahusiki na tuhuma hiyo.

 MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.