• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Nafurahishwa na Gymkhana kuinua vipaji vya mchezo wa golfu - RC MALIMA.

Posted on: June 8th, 2024



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema anafurahishwa na uwepo wa Gymkhana klabu ya  mchezo wa golfu Mkoani humo ambayo inawapa nafasi watoto kukuza vipaji vyao vya mchezo wa golfu na kuweza kutimiza ndoto zao kuwa wachezaji wakubwa wa mchezo huo.

Mhe. Malima amesema hayo Juni 8, 2024 wakati  wa maandalizi ya mashindano ya Alliance one  Morogoro Open Golfu ambayo yanatarajia kufanyia kuanzia Juni 14 hadi 16 mwaka huu katika viwanja ya Gymkhana vilivyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema kupitia programu hiyo ya kuinua vipaji vya golfu katika jamii  itaenda kuongeza chachu na thamani ya mchezo huo na utainua vipaji vya watoto hao katika jamii mbalimbali mkoani humo na nje ya mkoa.

".... Nafurahishwa sana na hiyo trend ya Gymkhana Morogoro  ya kuinua vipaji miongoni mwa watoto mbalimbali kutoka kwenye jamii ambao tunatarajia baadae wawe wachezaji bora  Afrika na Dunia kwa ujumla...." Amesema Mhe. Adam Malima.

Aidha, amewahakikishia washiriki wote wa mchezo huo uwepo wa usalama katika mashindano ya "Alliance one  Morogoro open 2024" wakati watakapokuwa katika Mkoa huo, pia amewashukuru wadhamini wote waliojitokeza katika kudhamini mashindano hayo na kupelekea kuwa chachu ya kufanikisha malengo yake.

Pia Mhe. Malima amesema ili kuboresha mashindano hayo zaidi kuna umuhimu mkubwa wa kuunganisha na Sekta ya utalii kwa sababu Mkoa wa Morogoro una vivutio vingi  ambapo washiriki kutoka katika sehemu mbalimbali baada ya kushiriki mchezo huo watapata fursa ya kwenda kuangalia vivutio ikiwemo mbuga za wanyama .

Naye Mwenyekiti wa Morogoro Gymkhana Club ambae pia ni Katibu wa Chama cha Golfu Tanzania Bw. Dickson Sika amewataka wanamorogoro na viunga vya jirani kuwapeleka watoto wao kujifunza mchezo wa golfu ambapo watafundishwa bure (Junior training ) pia ameishukuru sana Serikali ya Mkoa katika kufanikisha mashindano hayo yatakayofanyika hivi karibuni.


Kwa upande wake Kiongozi wa Morogoro Gymkhana Club upande wa wanaume Bw. Seif Mcharo amesema hadi sasa wachezaji zaidi ya 80 wamejisajili kwenye mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika ndani ya siku tatu na kuhusisha vilabu vya Tanzania  na nje ya Tanzania pia yatahusisha watoto.

MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.