• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano aagiza kutekeleza maagizo ya SADC.

Posted on: September 15th, 2021

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Balozi Fatma Mohammed Rajab ameagiza kufanyika haraka zoezi la mpango mkakati elekezi wa Jumuiya ya nchi zilizo kusini mwa Afrika - SADC wa mwaka 2020 - 2030 ili kutoa fursa kwa nchi wanachama kuandaa miradi na programu zitakazojumuishwa pamoja kwa lengo la kupewa fedha.

Balozi Fatma ametoa agizo hilo Septemba 15 mwaka huu kwa wajumbe wa Kamati tendaji wa Wizara mbalimbali wakati wa ufunguzi wa warsha ya kitaifa ya uwekaji gharama katika mpango mkakati elekezi wa maendeleo wa kanda ya SADC – Regional Indictive Strategic Development Plan - RISDP kwa mwaka 2020 – 2030 iliyofanyika katika Hotel ya Antique iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Amesema, zoezi la uwekaji gharama katika mpango wa utekelezaji wa RISDP ni maelekezo ya baraza la mawaziri wa SADC katika mkutano uliofanyika Agosti 2021 Lilongwe nchini Malawi, ambapo katika mkutano huo nchi wanachama zilielekezwa kutekeleza zoezi la kukamilisha maoni yao katika sekretarieti ya SADC kabla ya Septemba  30 mwaka huu.

‘’ jukumu hili sio jepesi na ni muhimu likachukuliwa kwa uzito wake na likamilike kama lilivyopangwa ili kuendelea kuilinda sifa hiyo ya Tanzania katika SADC’’ amesema Balozi Fatma.

Aidha, Balozi Fatma amesema lengo la mpango huo ni kuimarisha Ushirikiano katika Kanda kwa ajili ya kuharakisha juhudi za kupunguza umaskini na hatimaye kufikia malengo ya maendeleo ya kiuchumi na yasiyo ya kiuchumi.

Katika hatua nyingine, Balozi Fatma amebainisha maeneo matano muhimu ambayo mpango huu mpya wa SADC umejikita, maeneo hayo kwanza ni eneo linalohusu Amani, usalama na utawala bora, pili ni maendeleo ya viwanda na ushirikiano wa masoko, tatu ni maendeleo ya miundombinu katika kusaidia ushirikiano wa Kikanda.

Maeneo mengine katika mpango huo ni pamoja na maendeleo ya jamii na watu, tano ni kuhusu Jinsia, Vijana, Mazingira na Mabadiliko ya tabianchi na Usimamizi wa hatari ya Maafa na mwisho ni Usimamizi wa kimkakati wa Mpango Mkakati elekezi wa Maendeleo ya Kanda.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Agnes Kayola  amesema warsha hiyo inajumuisha washiriki kutoka Tanzania bara na Zanzibar ambao watakaa pamoja na sekretarieti ya SADC ili kukamilisha zoezi hilo kabla au ifikapo Septemba 30 mwaka huu.

Katika hatua nyingine, Balozi Kayola amesema Wizara ya mambo ya ndani ina wajibu wa kuhakikisha taasisi zote za Serikali zinashiriki kikamilifu kuweka gharama kwenye mipango ya kila sekta ambayo inatekelezwa na SADC ndani ya kipindi hicho cha 2020 - 2030.

Naye, Mshauri Mwelekezi kutoka Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika Dkt. Tumaini Katunzi amesema mpango huo ni shirikishi kwa wanachama wa Jumuiya ya SADC  ambao iwapo utatekelezwa utazibadilisha nchi hizo ziweze kufanya kazi kwa pamoja na kukuza rasilimali zilizopo katika nchi hizo.

Maandalizi ya Mpango huo mpya wa SADC unakuja baada ya Mpango wa awali wa Jumuiya hiyo wa mwaka 2015/2020 kumalizika muda wake huku Mpango huu mpya ukitekelezwa kwa kufuata Dira ya SADC ya mwaka 2020/2030


MWISHO.

Nb: Bonyeza link hapa chini kuangalia taarifa hii.

https://www.youtube.com/watch?v=Ag5A_sMPh6I

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.